Maaskofu wa Usccb,wadai COP28,kusikiliza kilio cha dunia&kilio cha Maskini
Na Angella Rwezaula, - Vatican.
Katika kulekea kilele cha Mkutano wa COP28 huko Dubai, ulifunguliwa tarehe Mosi Desemba 2023, Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Marekani walionya kwamba malengo ya hali ya tabianchi lazima yawakilishe 'kilio cha dunia' na 'kilio cha maskini'.(https://www.usccb.org/news/2023/cop-28-us-bishops-call-international-climate-policies-promote-justice).Kwa hiyo Maaskofu wa Marekani wamejiunga na wito wa kimataifa wa kuwataka viongozi zaidi ya 70,000 na washiriki katika COP28 unaoendelea huko Dubai kujitolea kuongeza kasi ya mabadiliko kutoka katika matumizi ya mafuta hadi nishati safi ili kudhibiti athari mbaya ya mabadiliko ya tabianchi, na kusaidia wale walio hatarini zaidi katika mchakato huo. Katika taarifa iliyotolewa usiku wa mkesha wa mkutano wa hali ya tabianchi wa Umoja wa Mataifa tarehe 30 Novemba 2023, Maaskofu wa Marekani walielezea uharibifu wa uchumi wa dunia, kupitia uingizwaji wa nishati ya mafuta na nishati salama, ya kuaminika, ya bei nafuu na safi, kama "changamoto kuu ya mazingira inayokabiliwa na mataifa yote." Kutoka Vatican ilitangaza kuwa Papa Francisko hataweza kuhudhuria mkutano huo huku akipata nafuu kutokana na mafua na maambukizi ya mapafu. Lakini suala la nishati ya mafuta limo kwa hakika katika moyo wa majadiliano.
Mkutano huo unatarajiwa kuwa wakati muhimu kwa aina fulani ya ahadi ya kukomesha upanuzi wa mafuta, na "kuondoa" uzalishaji uliopo ili kufikia lengo la Mkataba wa Paris wa 2015 wa kushikilia wastani wa joto la dunia hadi chini ya nyuzi 2 ikilinganishwa na nyakati za kabla ya viwanda. Kulingana na wanasayansi wa hali ya tabianchi, kuzidi 1,5 C kunaweza kuweka sayari kwenye mawimbi ya joto ya mara kwa mara na makali zaidi, ukame, mafuriko na hali nyingine mbaya ya hewa inayoathiri maisha ya mamilioni ya watu. Nchi zinazoendelea, pamoja na mashirika mengi ya kidini na mashirika ya kiraia, yametoa wito kwa mataifa huko Dubai kujitolea kumaliza kabisa makaa ya mawe, mafuta na gesi ambayo ni vichochezi vya msingi vya mabadiliko ya tabianchi. Nchi zinazozalisha mafuta zimependekeza "kupunguza" au kusitishwa kwa "mafuta yasiyopunguzwa ya mafuta" (ambayo yataruhusu kuendelea kwa matumizi na uzalishaji wa vyanzo vya mafuta ya kaboni pamoja na maendeleo ya teknolojia ya kukamata-na-utoroshaji hewa chafuni ili kuvuta uzalishaji wa hanga).
Taarifa ya Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani (USCCB) ilirejea Waraka wa Kitume wa hivi karibuni wa Papa Francisko 'Laudate Deum' (Msifuni Mungu) ( Apostolic Exhortation ‘Laudate Deum’) ambapo Papa aliwahimiza viongozi wa ulimwengu kuchukua hatua juu ya mabadiliko ya tabianchi wakati sayari inakaribia "hatua ya kutoweza kurudi. Mgogoro wa hali ya tabianchi ni fursa ya kupanga upya uhusiano wa kimataifa kuelekea manufaa ya wote ambapo nchi na jumuiya zinaweza kufanya kazi pamoja ili kufikia haraka kwa madhubuti mpito wa nishati, waliandika maaskofu huku wakinukuu waraka wa Papa uliochapishwa mnamo tarehe 4 Oktoba 2023 kabla ya mbele ya COP28. Maaskofu wa Marekani kwa hiyo walibainisha kuwa licha ya ukuaji mkubwa wa nishati mbadala duniani kote, mfumo wa uchumi wa kimataifa unabakia kuendeshwa na nishati ya mafuta. Maaskofu hao walikubali juhudi za hivi karibuni za uondoaji hewa chafuzi nchini Marekani, nchi ambayo ni mtoaji mkubwa zaidi wa gesi chafuzi duniani, kuelekeza uwekezaji wa kihistoria kuelekea miundombinu ya hali ya tabianchi na maendeleo ya teknolojia.
Hata hivyo, walionya kwamba juhudi zozote za kuhamia vyanzo vinavyoweza kurejeshwa hazitafanikiwa ikiwa zitaongeza kwa kiasi kikubwa gharama za nishati kwa wananchi wa kipato cha kati na cha chini, na bila msaada wa kifedha kutoka kwa mataifa yaliyoendelea kwa ajili ya kukabiliana na hali, ustahimilivu na ufufuaji wa watu wengi zaidi mazingira magumu kwa sababu ‘Kilio cha dunia’ na ‘kilio cha maskini kinasikika ulimwenguni. “Hakuna serikali itakayofanikiwa kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi kwa muda mrefu ikiwa itahitaji ongezeko kubwa la gharama za nishati kwa wananchi wa kipato cha kati na cha chini. Kwa maneno mengine, malengo ya hali ya tabianchi lazima yawakilishe ‘kilio cha dunia’ na ‘kilio cha maskini,’ na yajumuishe usaidizi wa kifedha kutoka kwa mataifa yaliyoendelea kwa ajili ya kukabiliana na hali, ustahimilivu, na kupona kwa walio hatarini zaidi. Haki kwa maskini, ikiwa ni pamoja na watu bilioni 3.3 duniani kote wenye nishati ndogo na milioni 700 bila umeme wowote, ni mtihani muhimu wa sera ya maadili ya tabianchi.”
Kwa mujibu wa Baraza la Maaskofu katoliki nchini Marekani (USCCB) wanaandika kuwa: Haki kwa maskini, ikiwa ni pamoja na watu bilioni 3.3 duniani kote wenye nishati ndogo na milioni 700 bila umeme wowote, ni mtihani muhimu wa sera ya maadili ya hali ya tabianchi ilihitimisha taarifa hiyo. COP28 itaendelea hadi tarehe 12 Desemba 2023. Mkutano huo kwa hakika inataka kufanya tathmini ya kwanza ya kimataifa ya makubaliano ya kihistoria yaliyofikiwa katika COP21 huko Paris. Katika siku ya ufunguzi mafanikio makubwa yalipatikana kwa kuzinduliwa kwa Mfuko wa Fidia ya Hasara na Uharibifu wa hali ya tabianchia uliotafutwa kwa muda mrefu, kufuatia makubaliano yaliyofikiwa na Wanachama mwaka 2022 katika COP27 huko Sharm el-Sheikh ili kusaidia nchi zinazolipa mzigo mkubwa wa mabadiliko ya hali ya tabianchi.