Tafuta

Vijana wengi, mapadre, maaskofu, watawa kike na kiume wako tayari nchini Ureno kuudhuria siku ya vijana duniani. Vijana wengi, mapadre, maaskofu, watawa kike na kiume wako tayari nchini Ureno kuudhuria siku ya vijana duniani. 

WYD,Lisbon 2023:Vijana wa majimbo 10 kati ya 15 nchini Ivory Coast wako tayari kwa WYD

Kila kona ya dunia,imetuma vijana wake ili kuwakilisha wengine katika siku ya vijana Duniani huko Lisbon 2023. Kutoka nchi ya Ivory Coast inawakilishwa na vijana kutoka majimbo 10 katoliki kati ya 15 nchini humo.Vijana hao wanasindikizwa na mkuu wa kijimbo wa Mashirika ya Kimissionari ya Kipapa (PMS) Yopougon.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Padre Régis Akpess ni mkuu wa kijimbo wa Mashirika ya Kimissionari ya Kipapa (PMS) huko Yopougon, mojawapo ya majimbo kumi ya Ivory Coast yatakayoshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani huko Lisbon kuanzia tarehe 1 -6 Agosti ambayo yanaongozwa na Kauli mbiu “Maria aliondoka akaenda kwa haraka” (Lk 1:39). Na ambaye akihojiana na Shirika la Habari za Kisionaria Fides kuhusiana na tukio hili muhimu alisema: “Wakati Askofu wangu, Jean Salomon Lezoutié, aliponiomba niandamane na vijana hadi Lisbon katika  Siku ya Vijana Ulimwenguni, nilikubali kwa shukrani na furaha kubwa!

Vijana wengi kabla ya Lisbon wamepitia Fatima
Vijana wengi kabla ya Lisbon wamepitia Fatima

Mmisionari wa Ivory Coast, ambaye ni wa  jimbo la Yopougon aliongeza kusema kuwa  “Sisi ni kundi la mapadre, watawa, vijana wa kike na kiume  kutoka majimbo  10 kati ya 15 ambayo  ni ya Kanisa la Ivory Coast. Tulifika Portimao, Ureno, Alhamisi tarehe 20 Julai 2023  na kisha tukaelekea Lisbon ambako tutakaa wiki moja tukisubiri Misa na Papa Francisko”, alieleza Padre Regis. Kwa kuongezea, “Katika mwaka huu vijana  walishiriki katika mikutano mbalimbali ya maandalizi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Kitaifa ya Mashirika ya Kimissionari ya Kipapa. Washiriki wote walijiandikisha kwa shauku kwa ajili ya Siku ya vjana (WYD) hii ambayo wanaiona kuwa tukio la ajabu la maombi na mikutano”.  Na zaidi alisema “Jimbo la  Yopougon lina kanisa lilip ha ambal linajumuisha takriban 45 harakati, makundi na vyama vya sala”. Kwa hiyo majimbo 10 yanayowakilisha katika Siku ya vijana (WYD) huko Lisbon ni yale ya: Abidjan, Yopougon, Bassam, Mtakatifu Pedro, Abengourou, Agboville, Katiola, Korogho, Daloa, na Bouaké.”

31 July 2023, 17:21