Tafuta

2022.11.03 Loredana Mantello akihojiana na mwandishi wa habari Vatican. 2022.11.03 Loredana Mantello akihojiana na mwandishi wa habari Vatican. 

Loredana Mantello,Papa anahamasisha maelewano

Loredana Mantello,mpiga picha wa Kiitaliano ambaye amekuwa akiishi Bahrain kwa miaka 18 iliyopita,amesema ziara ya Papa Francisko ni wakati wa muhimu wa kihisia kwa jumuiya katoliki wanaoishi nchini humo na kutafakari jinsi dini mbalimbali zinavyoweza kuishi pamoja kwa amani kama kaka na dada.

Na Angella Rwezaula, - Vtican.

Katika mahojiano na Mwandishi wa Habari   wa Vatican News,  Devin Watkins na Bi Loredana Mantello, mpiga picha wa Kiitaliano ambaye amekuwa akiishi Bahrein kwa miaka kumi na minane, alishirikisha mawazo yake kuhusu maana ya ziara ya Kitume ya Papa Francisko nchini humo. Licha ya kuwa mgeni katika mchi hiyo Bi. Mantello alisema kwamba ziara hiyo huko   Bahrein anaiona kama nyumbani kwake  yake, na kwakmba anajisikia kukaribishwa sana nchini humo. Mapenzi yake kwa nchi ya  Bahrein yanaoneshwa kila wakati.  Ikiwa ni ziara yake ya  kwanza ya Papa Francisko nchini, humo  Bi Mantello alibainisha  kwamba ni ya hisia kubwa sana kwake na kwa jamii nzima.

Bi Loredana Mantello akizungumza juu ya ziara ya Papa huko Bahrein
Bi Loredana Mantello akizungumza juu ya ziara ya Papa huko Bahrein

Ziara hiyo inadhihirisha jinsi nchi ilivyo wazi kwa dini zote, huku akisisitiza na mchango wa mfalme huyo kwa  kutoa ardhi ya kujenga Kanisa Kuu la katoliki la Mama Yetu wa Arabia alibainisha  Bi Mantello. Kanisa na msikiti katika Manama, ambao ni mji mkuu, alisema kwake ni kuwa  karibu sana  kimwili, kwani anapokuwa anakwenda kanisani, anauona hata msikiti na kuwa na hisia ya suala la  wote ni ndugu.

Ziara ya Kitume ya  Papa  Francisko huko Bahrein
Ziara ya Kitume ya Papa Francisko huko Bahrein

Papa Francisko yuko nchini Bahrein  tangu alhamisi tarehe 3 hadi 6 Novemba. Hii  ni ziara yake ya Kitume ya 39 kuwa nje ya nchi na nchi  ya 58 kutembelea akiwa kama Papa. Ziara hiyo inaongozwa na kauli mbiu ya kukutana na kutia moyo kwa Wakatoliki katika eneo hilo. Papa Francisko  kwa maana hiyo alipofika alikaribishwa na kutoa hotuba na wakati huo huo Ijumaa tarehe 4 Novemba 2022 ameudhuria sherehe za kufunga Kongamano la kwanza kabisa la Bahrain Forum for Dialogue: East and West for Human Coexistence, Yaani Kongamano la Bahrein kwa ajili ya Mazungumzo, Mashariki na Magharibi kwa kuishi pamoja, ambalo limeshuhudia takriban viongozi 200 wa madhehebu mbalimbali waliokusanyika ili kumasisha na kukuza udugu. Baba Mtakatifu Francisko ataendelea kuwa huko ili kuimarisha Imani kwa watu wa Mungu ambapo atarudi Roma mnamo Dominika tarehe 6 Novemba 2022.

Ziara ya Kitume ya  Papa  Francisko huko Bahrein
Ziara ya Kitume ya Papa Francisko huko Bahrein
Ziara ya Papa huko Bahrein
04 November 2022, 15:04