Tafuta

2022.06.27 Padre  Vitus Borogo wa Jumuiya Katoliki ya Chuo Kikuu cha Jimbo la Kaduna nchini Nigeria ameuawa 2022.06.27 Padre Vitus Borogo wa Jumuiya Katoliki ya Chuo Kikuu cha Jimbo la Kaduna nchini Nigeria ameuawa 

Ghasia nchini Nigeria:Padre Vitus Borogo auawa

Shirika la Kipapa la Kanisa Hitaji limetoa tangazo kuhusu mauaji ya Padre Vitus Borogo wa Jumuiya Katoliki ya Chuo Kikuu cha Jimbo la Kaduna nchini Nigeria.

Vatican News

Katika ukurasa wa twitter wa Shirika la Kipapa la Kanisa Hitaji, limetoa mwaliko wa kuiombea roho ya  Marehemu Padre Vitus Borogo, aliyeuawa  nchini Nigeria na watu wenye silaha kwenye shamba la Magereza, kando ya Barabara ya Kaduna-Kachia. Padre Vitus alikuwa Padre  wa jumuiya katoliki ya Chuo Kikuu cha Jimbo la Kaduna na kwamba haya ni mauaji ya pili nchini Nigeria na ya nne barani Afrika tangu Mosi Januari  2022.

Mnamo tarehe 19 Juni  watu wasiopungua watatu waliuawa na takriban watu arobaini walitekwa nyara katika shambulio dhidi ya waamini wa Kanisa katoliki la Mtakatifu Moses, Robuh, katika jimbo la Kaduna. Nchi hiyo ya Nigeria imetikiswa na mashambulizi ya kusikitisha kwa miezi kadhaa. Siku ya Jumapili tarehe 5 Juni 2022 waamini wapatao arobaini walipoteza maisha katika shambulio dhidi ya Kanisa la Mtakatifu Francis Xavier huko Owo, katika jimbo la Ondo, kusini magharibi mwa Nigeria.

27 June 2022, 16:15