Sri Lanka:Kard.Malcolm Ranjith ashutumu ubinafsi wa ulimwengu
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.
Katika Misa ya moja kwa moja iliyoongozwa na Kardinali Malcolm Ranjith, nchini Sri Lanka, misa iliyotangazwa na televisheni kwa mujibu wa habar za kanisa Asia UCA ameshauri waamini wa kila imani kujiomboa dhidi ya ubinafsi ili kuishi kwa mujibu wa misingi ya dini yao, ili kuzuia kwamba ulimwengu usiharibike. Kwa mujibu wake amesema “majanga yote haya ambayo tunajikuta tunakabiliana nayo katika jamii, kiukweli yamesababishwa na hisia zetu za ubinafsi”.
Kardinali Ranjith pia amezungumzia juu ya mashirika yenye nguvu na ambayo yanaendeleza kisiri siri, silaha za kibaiolojia kama vile silaha za maangamizi makubwa, aidha dini ambayo imesahauliwa katika nchi zenye uchumi mkubwa na kuwa na ukosefu wa kiroho na maadili. Kwa maana hiyo amesema “ haijalishi wewe ni dini gani, la muhimu ni kuishi kwa mujibu wa dini ambayo unaamini, katika ulimwengu huu ambao leo hii umejaa kizingiti cha uwiano mkubwa sana kati ya matajiri na masikini na ambao umezidi kuongezeka, wakati huo huo rasimali zake pia hazina usawa katika ugawaji na uchafuzi wa mazingira umesababishwa na ubinafsi wetu”. Amesisitiza Kardinali Ranjith.
Hata hivyo mbele ya kuongezeka kwa kesi za maambukizi ya covid-19, Serikali ya Sri Lanka imezuia mikutano ya umma hadi utaratibu mwingine utakapotolewa kwa maana hiyo vijiji vingi vimetengwa kwa ajili ya kupambana na wimbi la pili la virusi vya corona ambavyo vinasambaratika kwa haraka sana. Nchini Sri Lanka hadi sasa imerekodi zaidi ya kesi 17.300 na vifo 58. Kabla ya kuanza kwa wimbi la pili la maambukizi, wiki ya kwanza ya mwezi wa Oktoba walikuwa wameorodhesha kesi 3.396 na vifo vya watu 13 tu.