Tafuta

Maaskofu wa Uingereza na Walles wanasitika ongezeko la utoaji wa mimba nchini mwao Maaskofu wa Uingereza na Walles wanasitika ongezeko la utoaji wa mimba nchini mwao 

Uingereza:Ungereza yaongoza katika rekodi ya utoaji mimba

Uhamasishaji wa haraka na unashauriwa na maaskofu wa Uingerena mbele ya takwimu zilizotolewa kuhusu utoaji mimba nchini humo.Takwimu zinaonesha kuwa mimba zilizotolewa ni 109.836 kwa raia wa Uingereza na Walles katika miezi sita ya mwanzo wa mwaka kwa ongezeko la zaidi ya 4,000 kulinganisha na kipindi sawa cha mwaka uliopita 2019.

Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican

Huzuni kubwa na majuto ndiyo maoni yaliyotolewa na viongozi  wa Baraza la Maaskofu wa Uingereza na Wales kupitia tovuti yao, kuhusu idadi kubwa ya utoaji mimba ulioneshwa kwenye ripoti  Uingereza. Kwa mujibu wa  takwimu iliyochapishwa Juni iliyopita na Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii, utoaji mimba ni 109,836 uliofanywa kwa wakazi wa Uingereza na Weles katika miezi sita ya kwanza ya mwaka huu, ambayo inajumuisha kipindi  kutoka tarehe 1 Januari, hadi tarehe  30 Juni 2020 ikiwa na ongezeko  zaidi ya utoaji mimba elfu nne ukilinganishwa na kipindi kama hicho cha mwaka jana 2019.

Inasikitisha sana kwamba akina mama wengi wamehisi hawawezi kuendelea na ujauzito wao wanasema maaskofu , na ni matarajio yao kwamba wanaweza kupata msaada wa kweli wanaohitaji kupata watoto, bila kujali hali zao,.

Takwimu hiyo ni ya juu zaidi kuwahi kutokea nchini Uingereza, ambapo utoaji mimba umekuwa halali tangu 1967. Kwa mujibu wa taasisi ya Iona, ambayo inahamasisha jukumu la familia katika jamii  imefafanua kwamba utafiti huo ni wa  kushangaza kwani inamaanisha  kila watoto watatu  wanaozaliwa, mtoto mmoja hutolewa mimba.

19 September 2020, 16:48