Tafuta

Covid-19 Kenya Covid-19 Kenya 

KENYA:Murang'a:kliniki mpya ya Kiriaini ya Wamisionari wa Consolata!

Kanisa Katoliki nchini Kenya katika sekta ya afya na ambayo ina hamasisha zaidi kwa niaba ya walio maskini zaidi na walio katika mazingira magumu.Hospitali hiyo,kiukweli katika haraka zake kwa walio wa mwisho imezindua kitengo kipya.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Jitihada ya Kanisa Katoliki nchini Kenya katika sekta ya afya inajikita zaidi na zaidi wa ajili ya walio maskini na walio katika mazingira magumu zaidi. Hospitali ya Kiriani ya Wamisionari, imeweza kuzindua kitengo kipya ndani mwake. Katika hafla ya uzinduzi huo ilifanyika tarehe 17 Julai 2020, akiwepo Katibu wa Baraza la Waziri wa Afya, Mutahi Kagwe na aliyetoa  baraka ni  Askofu Joseph Ndembu Mbatia, mkuu wa Tume ya Maaskofu Kenya kwa ajili ya  Huduma ya kichungaji ya Afya. Pia alikuwepo Askofu James Maria Wainaina, Askofu wa Murang'a, ambapo hospitali hiko iko katika eneo lake.

Hospitali ya utume ya Kiriaini kwa mujibu wa habari kutoka Cisa wanasema, daima imekuwa mstari wa mbele kutoa huduma kamili za matibabu za kukinga na kulinda wote, kwa umakini zaidi na zaidi maskini ambao hawana fursa, katika roho ya kutangaza huduma ya uponywaji wa Kristo.

Utambuzi na Shukrani kwa kazi ya Kanisa umeoneshwa na Mutahi Kagwe, ambaye alikumbuka kwamba muundo wa hospitali hiyo ni mmoja ya hutoaji huduma kuu ya afya ya wenyeji wa eneo hilo. Kunako mwaka wa 2019, kwa ujumla wagonjwa 63,772 walitibiwa katika Hospitali ya Kiriaini. Mwakilishi wa serikali pia alisisitiza juu ya mamlaka ya huduma bora za afya kuhakikisha ufanisi mkubwa, upatikanaji na ukasi katika matibabu, ambao tayari utakuwa wa siku zijazo!

Hospitali ya Wamisionari ya Kiriaini ilianzishwa na Watawa shirika la  Wakonsolata kunako  1955 kama kiliniki ndogo. Kadiri ya siku   zilivyoongezeka na kuongeza kwa vifaa vyake ikawa ni kituo cha kwanza cha uzazi na baadaye  kuwa hospitali halisi  yenye vitanda na idara 72 za Wanajinakolojia na Uzazi, Madaktari wa watoto na upasuaji.Kwa sasa  hosptali hiyo inasimamiwa na jimbo la Murang'a.

29 July 2020, 12:47