Marekani:Ikiwa unataka amani fanya kazi kwa ajili ya haki!
Na Sr. Angela Rwezaula Vatican
Kufuatia matukio mabaya ya hivi karibuni ambayo yalisababisha kifo cha Floyd na kuwekwa mahabusu polisi na majadiliano ya kitaifa juu ya marekebisho ya polisi na haki za kikabila, nchini Marekani, Maaskofu wa Tume ya maaskofu kuhusiana na masuala haya kwa namna ya pekee mada hii kuu ambayo imetikisa mkubwa ulimwengini, hivi karibuni wametuma barua kwa wanachama wote wa Bunge la Marekani kwa kutoa tafakari na kanuni juu ya uwajibikaji wa polisi na mageuzi. Barua hiyo imetiwa sahini na Askofu Muu Paul S. Coakley wa mji wa Oklahoma, ambaye ni Rais wa Tume ya Haki na mandeleo fungamani ya binadamu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani (USCCB); Askofu Mario E. Dorsonville, Msaidizi wa Jimbo Kuu la Washington, Rais wa Tume kwa ajili ya wahamiaji na Askofu Shelton J. Fabre wa Houma-Thibodaux, Rais wa Tume ya kupinga ubaguzi wa rangi.
Katika barua ya maaskofu wanabainisha kuwa ingawa maafisa wa utekelezaji wa sheria hutoa huduma ili bora na muhimu lakini mauaji ya kutisha na yasiyofaa ya George Floyd, Rayshard Brooks na wengineo wengi yameonyesha kuwa lazima kuwe na mazoezi yaliyo muhimu ya mafunzo na uwajibikaji wa polisi, na kwa uhakika katika kurekebisha utumiaji wa nguvu iliyo mbaya, lakini pia hata katika kuondoa mifano ya ubaguzi na hukumu ili uwajibikaji wa kweli uweze kuthibitishwa kabla ya maisha mengine kupotea.
Maaskofu hawa katika barua yao inaonesha hata barua nyingine ya kichungaji juu ukiukwaji wa haki na juu ya ubaguzi wa umma uliojionesha katika mchakato wa maisha ya kihistoria nchini humo na zaidi kuangazwa na maoni ya Papa Francisko kuhusu kifo cha George Floyd, vile vile hotuba kuhusu matumizi mabaya ya nguvu kwa upande wa polisi na kutazama juu ya jukumu la polisi katika jamii kwa mtazamo wa ushauri wa Papa mstaafu Benedikto XVI na Papa Mtakatifu Yohane Paulo II.
Maaskofu hao wanasisitiza kuwa “tunahifadhi kwa muda refu utamaduni wa Mtakatifu Agostino, Mtakatifu Tomasi wa Aquino, na mchungaji Dk. Martin Luther King ambaye anasema kwamba “kusudi la sheria na utekelezaji wa sheria ni kukuza haki” . Kwa maana hiyo wanaongeza kusisitiza kuwa “Suluhisho moja la changamoto za wakati huu ni kufuata ushauri wa busara wa Papa Mtakatifu Paulo VI aliyesema kuwa 'Ikiwa unataka amani, fanya kazi kwa ajili ya haki”