Ufilippino#Coronavirus:Mpango wa kurudisha watu shambani bila uwekezaji mkubwa!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Dharura ya Coronavirus imesukuma serikali ya Ufilipino kuondoa mradi wa zamani wa maendeleo ili kuhimiza kurudi katika mashamba kwa kuwaondoa watu katika mitaa mibaya iliyojengwa nje ya mji mkuu Manila. Umasikini wa mashambani nchini Ufilipino ndiyo kweli sababu kuu ya uhamiaji wa ndani kutoka vijijini kwenda katika miji mikubwa kama mji mkuu huo, ambapo hata hivyo inaunda hali mpya mpya za kufurika kwa watu. Hii ni hali ambayo imejionesha zaidi wakati huu wa janga la virusi.
Kwa maana hiyo Rais wa Nchi Bwana Rodrigo Duterte ametangaza “Balik Probinsya, Bagong Pag-asa Program”, yaani Mpango wa kurudi katika wilaya mahalia”. Mpango huo umekubaliwa kwa shingo upande kutokana kwa maono ya Askofu Broderick Pabillo Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Manila na Msimamizi wa Kitume wa Jimbo hilo ambaye anakumbuka jinsi mipango mingi kama hiyo imeshindwa hapo awali kutokana na kukosekana kwa kazi watu wengi waliotumwa kurudi mashambani, na walirudi tena jijini.
Askofu Pabillo aliyeinukuliwa na shirika la habari la maaskofu Cbcpnews) “Sasa wanaahidi kuwapa mafunzo ya kitaalam na kuanza kuwapa mtaji ili kuwasaidia kukaa na hii ni matokeo chanya, lakini haitoshi. Kwa mujibu wa amebainisha kuwa ili mradi huo mpya ufanye kazi, serikali na biashara lazima ziwekeze pakubwa kwa kutoa ajira na huduma katika maeneo ya vijijini. Janga amsisitiza lihamasishe wito kwa Serikali ili waweke umakini sana katika sekta ya kilio ambayo hadi sasa ilikuwa imesahalika .“Kutengwa na kukaa ndani kwa mara nyingine kumedhihirisha jinsi wakulima na wavuvi ni muhimu katika uchumi wa Ufilipino na maisha yetu”.