Noeli ni kuonesha kwamba kila mtu ni mwenye thamani!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Kila mmoja wetu ni mwenye thamani na isiyoweza kubadilishiwa ndiyo wito unaoonekana katika Ujumbe wake wa Siku kuu ya Kuzaliwa kwa Bwana wa kwa waamini na awenye mapenzi mema wa Askofu Mkuu Anthony Fisher wa Sydney, nchini Australia. Siku kuu ya kuzaliwa kwa Bwana inaeleza kuwa sisi tunathamaniwa na tumependwa.Inawezekana kusema kuwa ni kuweka chumvi nyingi lakini ndiyo maana yake anathibitisha Askofu Mkuu Fisher Kuzaliwa kwa Yesu kwa hakika kunaonesha kuwa Mungu anapenda sana mtu hadi kufikia kugeuka kuwa mmoja kati yetu kwa ajili ya wema wetu. Hiyo ndiyo Habari Njema ambayo wakristo hawachoki kamwe kutangaza. Na ndiyo hicho kinachotamaniwa kwa ajili ya wema ambao unafanyika ndani ya familia, ya parokia, shuleni, hospitalini na katika utume wa umisionari wowote ule. Hiyo ndiyo Habari Njema ambayo wakristo wa nyakati zote hawachoki kamwe kutangaza. Na ndiyo hicho kinachotamaniwa kwa ajili ya wema ambao unafanyika ndani ya familia, ya parokia, shuleni, hospitalini na katika utume wa umisionari wowote ule.
Uharibifu wa misitu na vichaka nchini Australia
Hata hivyo katika ujumbe wake, Askofu Mkuu Fisher hakukosa kuenesha janga la na idadi kubwa ya moto ambao unaendelea kuangamiza sehemu kubwa ya Australia kwa kipindi sasa ambacho hadi sasa imeharibu karibia ekari elfu 200 za misitu na vichaka. Injili inahamasisha kuwa na jitihada zetu kwa ajili ya kuweza kusaidia kilimo na wale wote waliokumbwa na baa hili la ukame, amesisitiza; Injili inatia moyo na ujasiri wa kukesha dhidi ya moto naili kuweza kuwatunza wale ambao wanapambana mbele ya majanga haya. Mtoto Yesu kwa hakika anazungumza na kila mwanadamu kwa maana yeye alikuja kwa ajili ya mtu mwenyewe binadamu.
Kama ilivyokuwa kipindi cha Erode hata leo hii bado kuna watoto wasio na hatia
Askofu Mkuu wa Sydney katika ujumbe wake anatoa mwaliko pia wa kutosahau mauaji ya wale wasio kuwa na hatia ambao anasema kama ilivyokuwa kipindi cha Erode, hata leo hii bado watoto wanauwawa ambao hawajazaliwa. Leo hii ni hatari zaidi kuliko awali hasa baada ya uamuzi wa hivi karibuni wa utoaji wa mimba huko Wales Mpya ya Kusini; “Watoto wasio na hatia, walemavu na wasiohitajika; wanaokandamizwa bila hatia, kutiwa kwa ndani kwa Wakristo, wanaoteswa na kuwatia kizuizini wale wanaotafuta hifadhi; wazee wasio na hatia na kutunzwa vibaya huku wakitishiwa na euthanasia au kifo laini. Mbele ya mambo yote hayo, sherehe za Kuzaliwa kwa Bwana zinatoa fursa kwa mara nyingine tena kufanya uchaguzi kwa maana ya kutenda kama Erode yaani kuona kuwa kuna wale wanaostahili, au kutenda kama Malaika na wachungaji katika hori, waliotoa sifa kwa Mungu na kusali kwa ajili ya amani duniani kwa kuonesha kuwa kila maisha ya binadamu ni muhimu.