Rais wa zamani wa Afrika Kusini Bwana De Klerki amefariki akiwa na umri wa miaka 85
Na Sr. Angella Rwezaula – Vatican.
rRais wa zamani wa Afrika Kusini Bwana Frederiki de Klerk, ambaye pia alikuwa mhusika mkuu katika kipindi cha mpito cha taifa kuelekea demokrasia, alikuwa amegubduliwa na saratani mwaka huu, kulingana na msemaji wa Taasisi yake. Bwana de Klerk alikuwa mkuu wa nchi kati ya Septemba 1989 na Mei 1994. Mwaka 1990 alitangaza kumwachilia huru kiongozi aliyepinga ubaguzi wa rangi, Hayati Nelson Mandela, na kusababisha kura za vyama vingi mwaka 1994.
Taarifa kutoka mhusika wa rais huyo wa zamani Frederik de Klerk siku ya Alhamisi asubuhi tarehe 11 Novemba 2021 ilisomwa: “Rais wa zamani Frederick de Klerk alifariki kwa amani nyumbani kwake huko Fresnaye (Cape Town) mapema leo asubuhi kufuatia mapambano yake dhidi ya saratani ya mesothelioma.” De Klerk alitangaza kukutwa na maradhi ya saratani wakati wa kusherekea miaka 85 ya kuzaliwa kwake, mnamo tarehe 18 Machi mwaka huu.
Raii wa Zamani huyo anakumbukwa zaidi kwa hotuba yake maarufu aliyoitoa tarehe 2 Februari mwaka 1990, akitangaza kuondolewa marufuku dhidi ya chama cha African National Congress (ANC) na vyama vingine vilivyokuwa vinatetea ukombozi. Katika hotuba hiyo hiyo, aliamuru kuachiliwa kutoka jela kwa Mandela aliyekuwa akipinga ubaguzi wa rangi baada ya kifungo cha takriban miaka 27.
De Klerk na rais wa kwanza mweusi wa Afrika kusini Bwana Nelson Mandela walipata wote Tuzo ya amani ya Nobel mwaka 1993 kwa kuongoza mabadiliko makubwa kutoka kwa utawala wa wazungu walio wachache nchini humo.