2020.01.31 Anna Maria Tarantola,Rais wa Mfuko wa Centesimus Annus 2020.01.31 Anna Maria Tarantola,Rais wa Mfuko wa Centesimus Annus 

Tarantola:Kuamsha kuta hakusaidi,njia pekee ni ushirikiano kidugu

Rais wa Mfuko wa Centesimus Annus pro Pontifice Anna Maria Tarantola, amewakilisha Mkutano wa kimataifa wa siku siku mbili 21-22 jijini Vatican juu ya mapambano dhidi ya ukosefu wa haki,wa usawa na ubaguzi.Kuamsha kuta hakusaidii katu. Njia pekee ni ushirikiano kidugu.

Na Sr. Angella Rwezaula – Vatican.

Mshikamano, ushirikiano na uwajibikaji ndiyo mada inayoongoza kingamono la kimataifa la siku mbili 21-22 Oktoba ambalo limefunguliwa katika ukumbi mpya wa Sinodi Vatican na  litahitimishwa na kukutana na papa Francisko mnamo 23 Oktoba. Ni mambo msingi matatu ya matumaini ambayo Mfuko wa Centesimus Annus pro Pontifice, wameandaa katika tukio hili kwa kupitia kauli mbiu ndogo ya dawa kwa ajili ya kupambana na ukosefu wa haki, usawa na ubaguzi. Kwa maana hiyo mada hiyo ndiyo itakuwa ncha kali ya kukabaliana na watoa mada kutoka sehemu mbali mbali za ulimwengu  kama vile Mtuzwa nobel ya Fisikia 2018, Gérard Albert Mourou, na wakuu wa Vatican, miongoni  mwao akiwamo Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican, Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Vatican wa mahusiano na ushirikiano na Nchi, Kardinali Peter Turkson, Mwenyekiti wa  Baraza la Kipapa la Maendeleo Frangamani ya Binadamu.

Kuna majadiliano katika meza ya mduara  na mtazamo juu ya nyaraka za Papa Francisko za Fratelli Tutti na  Laudato si na ambazo kwa mujibu wa waandaji zinawakilisha mwendelezo wa kweli  wa mafundisho Jamii ya Kanisa katika historia. Kwa mujibu wa waandaji wamsema tuki la kongamano hili litahitiishwa na mkutano na Papa Francisko kwa washiriki wote. Lengo la tukio hilo ni kutathimini kwa dhati ikiwa wanaweza kujikita kwenye mazoezi ya thamani za mshikamano, ushirikiano na uwajibikaji, kutokana na  maelezo ya Bi Anna Maria Tarantola, Rais wa Mfuko wa Centesimus Annus pro Pontifice. Na thmani msingi  za  kukabiliana kwa dhati katika changamoto zote ambazo leo  zipo mbele  yak ila mmoja, kwa mfano kiafya kichumi kidigitali na kiikolojia ulimwenguni.

Mabadiliko ya tabiachi yanahitaji uongofu wa wote kwa maana kuna mtindo ndani mwake wa  kibiashara, kiuongozi katika misingi miwili ya elimu na mawasiliano. Bi Tarantola aidha amesebainisha kuwa lakini ni mabadiliko ambayo hayawezi kutimizwa bila kuwa na nanga za ushirikiano, mshikamano na uwajibikaji. Hii yote imejionesha katika tukio la kidunnia la janga la UVIKO kwamba bila kujiweka katika matendo, thamani hizi zinakosa njia na hakuna matokeo mema, lakini kwa kuunganisha misingi hiyo mitatu matokeo ni makubwa mno. Bi Tarantola amesema kuwa mabadikio  hata hivyo yanapaswa yawe ya mzunguko  kauanzia juu kwenda chini, kulia na kushoto kwa maana wote ni wawajibikaji. Ametoa mfano kuhusu  kijana mdogo Greta Thunberg: kwamba vijana walianzia chini na wako wanaendelea  kwa kasi kubwa lakini inayohitaji utambuzi wa kweli wa hali ya juu kwa kwa viongozi na ambayo ni muhimu sana, kwani kuamsha kuta hakusaidii katu, kinachotakiwa ni ushirikiano na mshikamano kwa wa kidugu na ambao unaweza kuoka sayari yetu.

21 October 2021, 17:42