Papa Francisko na Rais wa Baraza la Ulaya,Charles Michel Papa Francisko na Rais wa Baraza la Ulaya,Charles Michel 

Papa akutana na Michel:katika mazungumzo niwakimbizi wa Afghanis

Papa amempokea Rais wa Baraza la Ulaya na katika mazungumzo yao wamegusia masuala ya siasa kimataifa na kikanda.Baadaye amekutana na Katibu wa Vatican Kardinali Parolin akiambatana na Katibu wa Vatican kwa ajili ya Uhusiano na Ushirikiano na Nchi,Askofu Mkuu Gallagher.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Siasa za kimataifa na za kikanda, hasa kwa hali ya nchi ya Afghanistan, na baadaye changamoto za Ulaya ndizo zimekuwa mada muhimu katikati  ya mazungumzo kati ya Baba Mtakatifu Francisko na Rais wa Baraza la Ulaya, Bwana Charles Michel, ambaye amepolkewa katika Jumba la kitume Vatican. Bwana Michel, baada ya mkutano  na Papa  vile vile amekutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican akiambatana na Askofu Mkuu  Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na Ushirikiana na Nchi.

Rais wa Baraza la Ulaya akiwa na Kardinali Parolin Katibu wa Vatican
Rais wa Baraza la Ulaya akiwa na Kardinali Parolin Katibu wa Vatican

Wakati wa mazungumzo yao yamekuwa mazuri kwa mujibu wa taairfa kutoka Ofisi ya Wanahabari Vatican  na kwa maana hiyo masuala kadhaa ya siasa za kimataifa na za kikanda zilijadiliwa, kwa kuzingatia hali ya wakimbizi wa Afghanistan. Vile vile wakiendelea na mazungumzo hayo wamekuwa na mtazamo wa Mkutano juu ya mustakabali wa Ulaya  unaotarajiwa.

11 September 2021, 13:31