Mons.Duffe:kuishi,maelewano na uumbaji,dira na changamoto kwa ulimwengu wa leo
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.
Tangu Julai, Monsinyo Bruno-Marie Duffé, kuhani wa jimbo katoliki la Lyon, amemaliza muda wake wa jukumu kama katibu wa Baraza ka Kipapa la Maendeleo fungamani ya Binadamu,inayoongozwa na Kardinali Peter Turkson.Utume ambao ulianza mwezi Juni 2017 kwa kuteuliwa na Papa na utume ambao uliona hatua zake muhimu za kutumwa kwenda Brazil mnamo 2019 huko Brumadinho,baada ya kuanguka kwa mgodi wa chuma uliosababisha vifo vya zaidi ya watu 270.
Hata hivyo ukaribu na kurudiana ndiyo maneno muhimu katika mizani ambayo Monsinyo Duffé amekuwa akijikita nayo kufuatilia kwa miaka hi ina ambapo katika mahojiano na wafanyakazi wa wahariri wa idhaa ya kifaransa ya Vatican News,amesisitiza huku akilenga nyakati za kisasa ambazo anazifafanua kuwa zinaashiria changamoto kubwa ya kuishi pamoja, kutambuliwa na kukubalika na ambayo inatuweka kwenye kuegemea karibu kati ya vurugu na kupasuka “au” mazungumzo na kutiana moyo”.
Kuishi pamoja na ukarimu: changamoto kubwa za nyakati za kisasa
Sehemu kubwa ya shughuli yake imekuwa kwa miaka ya hivi karibuni na shida ya kiafya kwa sababu ya janga na chaguo la Papa la kuanzisha Tume ya COVID-19. Uzoefu ambao umeonesha na Monsinyo Duffé kwa uwazi kabisa ni kiasi gani afya, ekolojia na masuala ya kijamii yameunganishwa sana na kurudisha yale yaliyooombwa na Papa Francisko, ambapo yeye alitaka kurudishwa kwa upya kazi ya uumbaji. Na wahusika wote, maeneo yote, dini zote, ni muhimu kwa maana hii, kila mtu anaweza kuchangia kujenga, upya na kufunya hali mpya ya uhusiano kati yetu na njia mpya ya mazungumzo kati ya wote kwa kuunga mkono kazi ya uumbaji
Kumbukumbu ya maadili, dira ya kutoa kwa kila mtu
Lakini jinsi ya kutekeleza na ni wapi pa kuanzia, Monsinyo Duffé, pia akinukuu uzoefu uliopatikana Amerika Kusini, ameangazia dhana ya kumbukumbu, ya kutazama tena kumbukumbu zetu. Katika kumbukumbu zetu za pamoja na za kibinafsi tuna idadi kadhaa ya vitu ambavyo vinaweza kutusaidia kufikiria juu ya mtindo huu mpya. Sio ombi la kurudia mambo ya zamani, lakini kwa kupitia tena maadili na marejeo tuliyonayo ili kuanzia kupata tena maana ya"kikomo na mwendendo katika enzi ambayo Monsinyo Duffé anathibitisha inahitaji mabadiliko ambayo ni moja ya changamoto za leo ni hii. Kumbukumbu, tumaini, mshikamano thabiti - - ni kama dira ambayo tunaweza kutoa kwa kila mtu amesisitiza
Mageuzi ya Vatican: sio kanuni tu bali utambulisho wa Kanisa
Hatimaya, mawazo yake ni juu ya mageuzi yaliyoanzishwa na Papa, ambayo, mbali na kuwa ya kimuundo tu au ya kiutawala au hata ya kawaida, inapaswa kueleweka kwa maana ya mienendo ya utume na uwepo wa Kanisa katika ulimwengu wa kisasa. Picha ambayo mchungaji huyo anachukua ni ile ya ufunguzi wa Kipapa wa “njia na mitazamo ili wote waliobatizwa wawe wahusika katika utume huo. Sisi ni Kanisa katikati ya ulimwengu wenye wasiwasi, wakati mwingine hata huzuni. Sisi ni Kanisa ambalo limeitwa kuwapa watu uwepo, umakini, huruma na utunzaji. Na hii ndiyo maana ya mageuzi haya” amehitimisha mahojiano hayo Monsinyo Duffe.
Utume mwingine aliofanya
Monsinyo Bruno Marie Duffé alizaliwa huko Lyon (Ufaransa) mnamo tarehe 21 Agosti 1951. Mnamo Juni 1981, alipewa daraja la ukuhani katika Jimbo kuu la Lyon na akafanya huduma yake kama Paroko msaidizi na pia Paroko wa Parokia. Alipata Udaktari wake katika Falsafa ya Kisiasa na Maadili ya Jamii (1996). Kuanzia 1982 alikuwa Profesa wa Taalimungu ya Maadili na Mafundisho Jamii ya Kanisa, katika Idara ya Taalimungu katika Chuo Kikuu Katoliki cha Lyon na Kituo cha Wajesuiti cha Baume-Les-Aix; na tangu 2005 alikuwa Profesa wa Maadili Jamii na Afya huko Léon Bérard, Kituo cha Saratani cha Mkoa wa Lyon. Ni mwanzilishi mwenza na Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki za Binadamu ya Chuo Kikuu Katoliki cha Lyon (1985-2004), ambaye alichangia kikamilifu kuundwa kwa Mwenyekiti wa UNESCO juu ya haki za watu walio wachache, na alikuwa Mshauri wa Kanda ya Wafanyabiashara wa Kikristo na Wakurugenzi (EDC ).
Monsinyo Duffe amekuwa Mchungaji Kitaifa wa Jumuiya ya Wakatoliki wa Kanisa wa Faim et pour le Développement (CCFD Terre Solidare), Mwanachama wa Baraza la Haki na Amani la Ufaransa na Mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Vyeti cha Huduma ya Afya ya Kichungaji, katika Chuo Kikuu Katoliki cha Lyon, kwa malezi ya wachungaji wa hospitali na wale wanaohusika na huduma za afya ya kichungaji. Vile vile ni mwandishi wa machapisho juu ya mada ya haki za binadamu, na alishiriki, kama mtaalam katika uwanja huu, katika tume nyingi za kimataifa na agizo la Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu (OHCHR) na kwa Wakimbizi (UNHCR) , kwa kushirikiana na Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) mbali mbali , pamoja na: Caritas, Terre des Hommes, na Madaktari wasio na Mipaka. Tangu Juni 2017 amekuwa akihudumu kama Katibu wa Baraza la Kipapa la kuhamasisha maendeleo fungamani ya Binadamu.