2021.05.06 Rais wa Shirikisho la Uswisi Bwana Guy Parmelin 2021.05.06 Rais wa Shirikisho la Uswisi Bwana Guy Parmelin 

Papa Francisko amekutana na Rais wa Shirikilisho la Uswisi

Kukuza uhusiano mwema uliopo na ushirikiano na masuala msingi ya kimataifa ndizo zilikuwa mada ambazo zimegusiwa wakati wa mkutano wa viongozi hawa wawili jijini Vatican kati ya Papa Francisko na Bwana Guy Parmelin,Rais wa Shirikisho la Uswisi.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican.

Katika siku ya kuapishwa kwa Walinzi wa Uswisi, Alhamisi asubuhi tarehe 6 Mei 2021 jijini  Vatican, Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Rais wa Shirikisho la Uswisi, Bwana Guy Parmelin. Wakati wa mkutano wao, kwa mujibu wa msemaji wa vyombo vya habari Vatican kwa waandishi wa habari wamekumbushana kuhusu huduma ya ukarimu ya Walinzi wa Kipapa wa Kiswisi. Kwa njia hiyo, pua uhusiano mzuri na ushirikiano uliopo na wenye matunda kati ya Vatican na Shirikisho la Uswisi hasa kwa kutazama masuala makuu ya kimataifa na maeneo yenye masilahi ya pamoja katika mwaka wa mia moja tangu kuanza tena kwa uhusiano wa kidiplomasia.

Mara baada ya mkutano  huo pia Rais wa Shirikisho la Uswisi amekutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican akifuatana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa Kimataifa mjini Vatican.

06 May 2021, 17:31