Papa atembelea Jumuiya ya Baraza la Kipapa la Mawasiliano Vatican
Papa Francisko ametembelea Jumuiya ya Baraza la Kipapa la Mawasiliano Vatican,Jumatatu tarehe 24 Mei 2021 katika fursa ya maadhimisho ya miaka 160 ya Gazeti la Osservatore Romano na miaka 90 ya Radio Vatican.Zifuatazao ni habari fupi kwa njia ya picha za matukio
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Imekuwa furaha kubwa kwa lisaa limoja kwa Jumuiya ya Baraza la Kipapa la Mawasiliano kutembelewa na Papa Francisko, Jumatatu tarehe 24 Mei 2021. Ni katika fursa ya maadhimisho ya miaka 160 ya Gazeti la Osservatore Romano na miaka 90 ya Radio Vatican. Katika fursa hiyo Papa amefanya mkutano, amesali sala katika kikanisa kidogo kilichomo ndani ya jengo na amezungumza katika studio. Aidha amezungumza na rais wa Baraza la kipapa la Mawasiliano, mhariri mkuu, wakurugenzi wa idara na hatimaye wawakilishi wa waandishi wa Radio Vatican katika Ukumbi wa Marconi. Zifuatazo ni habari za picha kwa ufupi:
24 May 2021, 13:31