Kard Parolin kuwakilisha Papa huko Strasburg,kwa mia 1300 tangu kifo cha Mt.Odile
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.
Baba MtakatifuFrancisko amemteua Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican kuwa mwakilishi wake ili kushiriki maadhimisho ya Ekaristi takatifu ambayo itafanyika tarehe 4 Julai 2021 katika Kanisa Kuu la Strasburg, katika fursa ya miaka 1300 tangu kifo cha Mtakatifu Odile, Msimamizi wa Alsace.
Mtakatifu Odile, Msimamizi wa Alsace
Alizaliwa kwenye mwaka wa 660 na kifo chake mnamo mwaka 720, ambapo jina la mtakatifu Odile linamaanisha “ mwanga wa Mungu”, na alikuwa anatoka katika familia nzuri ya Wamerovingian. Akiwa kipofu tangu utoto wake , aliponywa kimiujiza wakati wa Ubatizo wake, alioupokea akiwa na miaka 15. Baadaye akawa mtawa na kuanzisha monasteri katika Jumba la kifalme la Hohenbourg, lililoko kwenye mlima ambao baadaye uliitwa jina lake, Mlima wa Mtakatifu Odile na ambao kiukweli ni mahali maarufu kwa hija na utalii huko Alsace. Alitangazwa kuwa mtakatifu na Papa Leo IX katika karne ya 11, na alitangazwa kuwa msimamii wa Alsace na Papa Pius XII mnamo 1946, mwaka mmoja baada ya kumalizika kwa Vita vya pili vya Kidunia ambavyo vilijaribu sana eneo hilo, lililounganishwa na Ujerumani wa Nazi. Kuanzia tarehe 13 Desemba 2020, Jimbo katoliki la Strasbourg limezindua Jubilei Kubwa ya maadhimisho ya miaka 1300 tangu kifo cha Mtakatifu Odile.
Umaalum wa udini wa Alsace
Jimbo la Strasbourg, kama vile jimbo jirani la Metz, lina umaalum wa kutumia sheria za makubaliano ya Kinapoleon. Makuhani wanalipwa na serikali na maaskofu walioteuliwa kwa pamoja na Papa na Rais wa Jamhuri, na kuchapishwa katika Jarida la Ofisi. Majimbo haya mawili kwa makubaliano yalikuwa yametembelewa na Mtakatifu Yohane Paulo II mnamo 1988. Kwa upande wake, Baba Mtakatifu Francisko alifanya ziara fupi huko Strasbourg mnamo Novemba 2014, kwa kufanya hotuba mbili katika Bunge la Ulaya na Baraza la Ulaya.