Mwenyeheri Pius IX Mwenyeheri Pius IX  Tahariri

Chanjo kwa wote,chanjo kwa maskini:mfano wa Pio VII&Pio IX

Kutazama historia ya upapa inatusaidia kuelewa maneno na ishara za Papa Fransisko, katika jitihada za kutoa na kuhakikisha kuwa chanjo inapatikana kwa wote kwa mfano halisi wa chanjo ya watu wasio na makazi Vatican.

Ilikuwa mwaka 1822, Edward Jenner, baba wa chanjo ya kisasa kupitia chanjo ya ndui, alikuwa bado hai wakati kampeni kubwa ya chanjo ilifanywa katika Serikali ya kipapa wakati huo ikiongozwa na Papa Pius VII, na alikuwa akihimiza sana na kuandaliwa kwa uangalifu na agizo lililotiwa saini na Katibu wa wakati huo wa Vatican Kardinali Ercole Consalvi. Moja kati ya Kanisa Katoliki na utunzaji wa kuzuia magonjwa ya mlipuko na ya majanga ni muungano wa kizamani: kwa Ni katika mtazama wa  historia inatuwezesha kuweka vizuri kile ambacho Baba Mtakatifu Francisko alisema juu ya chanjo dhidi ya Covid-19 na kile alichotekeleza kwa kupendelea upatikanaji wa chanjo hiyo kwa maskini na wasio na makazi. Watu walio katika foleni ya ukumbi wa Paul VI, wakisindikizwa na Kardinali Konrad Krajewski, Msimamizi wa Sadaka ya Kitume ya Papa kwa kuwakaribisha yeye binafafi kama Askofu wa Roma ni shukrani kubwa hata kwa zawadi ndogo ya chakula mabo ambayo yanawakilisha kwa dhati habari mpya.

Ndivyo anaandika Dk. Andrea Tornelli Mhariri wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano Vatican. Kati ya mwisho wa karne ya kumi na nane na mwanzo wa karne ya kumi na tisa, ukuaji wa janga la ndui huko Ulaya ulikuwa wa kutisha. Mnamo 1820, katikati ya nchi ya Italia kulikuwa ndiyo kitovu ja janga hilo. Papa hakusimama na kutazama tu. Katibu wa Papa Pius VII, wa waakti huo, katika kifungu cha sheria cha tarehe Juni 20 1822 na ambacho hivi katibuni kimetolewa maoni na Marco Rapetti Arrigoni juu ya breviarium.eu, aliandaa kampeni ya chanjo kutokana na kwamba Papa alikuwa ameamuru kuwepo chanjo katika serikali yake.

Ni jambo la kufurahisha kusoma mwanzoni mwa hati hizo na ambazo ni mada ya sasa kwa maneno yaliyokuwa yanahusu ndui ambayo kwa bahati mbaya hudhoofisha mtu na kuondoa maisha yake [...] na uingiza sumu zake za spishi za wanadamu kana kwamba ni kuiangamiza wakati wa kuzaliwa kwake. Mawazo haya ya kusikitisha sana, kila wakati yaliongezewa nguvu na kuzidishwa na mauaji ya mara kwa mara ya ugonjwa huo, na ambayo yalilazimisha  kuwashawishi kila watu kukumbatia kwa shauku ya kupendeza na kufanya chanjo  kwa shukrani  kwa njia rahisi ambayo ni sawa sawa katika kupunguza sumu  ya nguvu ya ugonjwa.

Nakala moja inayohusu chanjo iliyo chapishwa na Vatican ya karne mbili zilizopita inafafanua chanjo hiyo kama zawadi kutoka kwa Mungu, na mikakati ya  nguvu kama hizo zilizowekwa kama na upatikanaji  kwa Upendo wa Baba kuokoa watoto katika mwanzo wa maisha  na wakati zaidi hufanya kitu cha utunzaji wake kwa upendo, na katika kuhakikisha matumaini ya familia na ya nchi, kwa hakika kutarajiwa kwamba mara tu vikwazo vikishindwa ingeenea kila mahali kwa haraka zaidi . Hata wakati huo, hata hivyo, vipingamizi vilizuia maisha kuokolewa. Lakini haikuwa hivyo  kwani  misimamo ya hukumu ilikuwa na nguvu zaidi kwa wazazi wengine kuliko upendo wa uzao wenyewe.

07 May 2021, 19:58