24 .04.2021: SR. ALESSANDRA SMERILLI NI KATIBU MPYA MSAIDIZI WA KITENGO CHA IMANI NA MAENDELEO CHA BARAZA LA KIPAPA LA MAENDELEO FUNGAMANI YA BINADAMU 24 .04.2021: SR. ALESSANDRA SMERILLI NI KATIBU MPYA MSAIDIZI WA KITENGO CHA IMANI NA MAENDELEO CHA BARAZA LA KIPAPA LA MAENDELEO FUNGAMANI YA BINADAMU 

Sr. Smerilli ni Katibu Maidizi wa Maendeleo Fungamani ya Binada

Sr.Alessandrea Smerilli ni mwanauchumi na mwanashirika wa Mabinti wa Maria Mwombezi aliyeteuliwa leo hii na Papa kuwa Katibu Msaidizi wa Kitengo cha Imani na Maendeleo cha Baraza la Kipapa la Maendeleo Fungamani ya Binadamu.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Papa Francisko amemteua Katibu Msaidizi wa Kitengo cha Imani na Maendeleo cha Baraza la Kipapa la Huduma ya Maendeleo Fungamani ya binadamu, Sr. Alessandra Smerilli, F.M.A., Mwanashirika wa Mabinti wa Mama Maria Mwombezi wa Don Bosco, ambaye ni Profesa wa kawaida wa Uchumi wa sera za kisasa katika Chuo Kikuu cha Elimu ya Sayansi cha Roma.

Sr. Alessandra Smerilli, F.M.A., alizaliwa mnamo tarehe 14 Novemba 1974 huko Vasto (CH), Italia.  Alipata shahada ya udaktari wa Uchumi wa siasa katika Kitengo cha Uchumi cha Chuo Kikuu La Sapienza  Roma. Baadaye aliendelea na masomo ya stashahada ya Uchumi katika  Chuo Kikuu cha Anglia Mashariki ya Nowrich nchini Uingereza.

Pamoja na hayo,  amekua akijitoa katika jitihada za Kanisa ambalo lilimpelekea kuwa sehemu ya Kamati ya Sayansi na mratibu wa Wiki za kijamii za Wakatoliki na  tangu 2019 amekuwa mshauri wa  Vatican vile vile  tangu Machi 2020 mratibu wa Kikosi Kazi cha Uchumi cha Tume ya Vatican ya Covid-19, iliyoanzishwa na Papa Francisko. Miongoni mwa vitabu vyake alivyoandika ni: Mwanamke mchumi. Kutoka katika mgogoro msimu mpya wa matumaini”.

Akihojiwa na Vatican New, kuhusiana na uteuzi huo anasema alivyoshangaa kidogo na uteuzi kwa sababu amesema kwamba  alikuwa amekuja kufanya kazi hapo katika ukumbi wa wakala kama mshirika wa Tume ya Covid-19. Alidhani ni kazi ya muda mfupi lakini kadiri ya siku ndivyo imeleta mshangao huo. Katika kufanya kazi hapo amegundua ni  jinsi utume huo ulivyo mzuri wa Baraza hilo na jinsi gani linavyofikia ulimwengu wote. Yeye anahisi kutoa shukrani kwa Baba Mtakatifu na kwa Rais wa Baraza lake hilo, Kardinali Peter Turkson, aidha kwa wale wote wanaofanya kazi katika Baraza la Kipapa hilo  ambao wameonesha kupendezwa na kumwamini. Anatumainia kuwa ataweza kufanyanao katika sehemu yake ipasavyo.

24 March 2021, 17:21