Vatican:Ufisadi ni hatari kwa amani na usalama!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Mapambano dhidi ya ufisadi ndiyo ilikuwa mada msingi katika hotuba ya Mwakilishi wa Vatican katika Mkutano wa Jukwa la Kiuchumi na Mazingira wa Shirika la Usalama na Ushirikiano wa Ulaya (OSCE) katika jiji la Praga. Hotuba iliyokabidhiwa tarehe 10 Septemba 2020 ya Askofu Mkuu Charles Balvo, Balozi wa Kitume katika Jamhuri ya Ceca na Mkuu wa uwakilishi wa Vatican katika mkutano huo, inasema ufisadi ni hali halisi hatari kwa ajili ya amani na usalama. Katika hotuba hiyo bado wasiwasi ni mkubwa kutokana na kwamba fedha nyingi zilizotolewa kwa ajili ya kukabiliana na janga la Covid-19, tayari zimekwisha vutiwana kuwindwa katika shughuli za kihalifu na kusababisha hatari kwa wale ambao ni wenye kuhitaji zaidi ya fedha hizo na wanabaki bila msaada unaohitajika. Ni lazima kuwa waaminifu, Vatican inasisitiza kwa kuwa na utambuzi kuwa ufisadi unaweza kudhibitiwa kwa viwango vyovyote katika kila nchi mwanachama wa OSCE, na kwa maana ya kutambua uwepo wa jeraha kubwa kama hili ni wazi wa kuwa na uwezo wa kupambana nao.
Suluhisho inayolenga faida ya wote
Kutokana na hoja hiyo ni mwaliko kutoka Vatican wa kutafuta suluhisho jipya na bunifu katika muktadha wa sasa wa janga la corona au suluhishi ambazo hazina mgawanyiko, kisiasa au kuwanyika sehemu, lakini ambalo hutafuta kwa dhati kwa ajili ya faida ya wote na maendeleo fungamani ya wanadamu. Kwa kuzingatia hayo Vatican inakumbusha kuwa, kunako tarehe 1 Juni 2020, Papa Francisko alitangaza Hati yake ya ‘Motu poprio’ kuhusu sheria juu ya uwazi, udhibiti na ushindani katika taratibu za utoaji wa mikataba ya umma ya Vatican na Serikali ya Jiji la Vatican, kwa lengo la kupunguza kwa kiasi kikubwa hatari ya ufisadi wa wale ambao wameitwa kutawala na kusimamia vyombo vya Vatican. Kwa mujibu wa maandishi ya Askofu Mkuu Balvo aansema “Uamuzi huu wa Baba Mtakatifu, unapeleka kutambua kuwa jeraha la ufisadi, ambalo ni ukweli kwamba wakati wafanyakazi wa umma wanaiba au wanafuja fedha za umma, yote haya yanaathiri jamuiya wanazozihudumia ”.
Uwazi katika usimamizi wa mambo ya umma
Ikiwa kwa hakika usimamzi wa mambo ya umma yanakuwa wazi na uwajibikaji, maendeleo ya uchumi thabiti na wa kudumu na usalama, kwa dhati haviwezi kuwa mashakani, au hata ubatiri. Kwa maana hiyo Askofu Mkuu Balvo anatoa ushauri wa kupingana na ufisadi kwa njia ya utamaduni, elimu, mafunzo, ushiriki wa dhati wa kizalendo, kwa sababu anasema sheria ni za lazima, lakini hazitoshi. Kinachohitajika ni kutenda kwa ujasiri ili kukung’utua dhamiri nafsi, ili sintofahamu zilizoelezwa, ziweze kupitia na kufikia ushiriki kamili wa kutatua hali ngumu ya matukio haya kwa namna ya kupambana nayo.