Papa Francisko awatembelea  washiri wa michezo ya kiangazi mjini Vatican Papa Francisko awatembelea washiri wa michezo ya kiangazi mjini Vatican  

Papa Francisko awatembelea watoto katika michezo ya kiangazi mjini Vatican!

Tengenezeni marafiki,jifurahisheni pamoja maana mtu ajifurahishaye peke yake ni mbinafsi.Ndiyo ushauri wa Papa aliowambia asubuhi tarehe,20 Julai alipokutana na watoto wadogo na viongozi wao ambao tangu mwanzo wa mwezi huu wanashiriki michezo ya vijana kipindi cha kiangazi mjini Vatican.Papa amewasalimia wakati wanakunywa chai na kujibu maswali yao.

Na Sr. Angela Rwezaula- Vtivan

Watoto wengi walikuwa bado hawajaamini kumwona Papa anatokeza ambao kila aasubuhi wanakusanyika pamoja katika kituo cha kiangazi kilichopendelewa na Papa mwenyewe mjini Vatican kwa ajili ya kuwasaidia wazazi ambao wanafanya kazi mjini Vatican. Kiukweli ilikuwa ni baada ya saa tatu hivi, Papa Francisko amewatembelea watoto na vijana ambao walikuwa wanafungua kinywa katika uwanja wa Jengo la Papa Paulo VI.

Kwa mujibu wa msemamji Mkuu wa vyombo vya habari Vatican, Dkt. Matteo Bruni amesema “Mara baada ya kupitia kwenye meza zao, Papa ametembelea hata sehemu zote na maeneo yaliyotengeneza kwenye Ukumbi wa Papa Paulo VI  kwa ajili ya tukio hilo na kukaa katikati na washiriki  hao baadaye amerudi katika Makao yake ya  Mtakatifu Marta  saa nne na kuwashukuru kila mmoja wa wahudumu hao kwa kazi yao wanayotenda”. Wakati wa ziara yake hiyo fupi Papa Francisko amekaa katikati ya watoto na kuwatia moyo ili watengeneze marafiki wapya. “watu ambao hutaka kujifurahisha peke yao, mara nyingi ni wabinafsi, kwa maana ni lazima kukaa pamoja na marafiki”, Papa amebainisha.

Padre Fontana aeleza furaha na mshangao wa watoto

Akiwasalimia watoto, Papa amepitia katika meza zao kuanzia zile za  watoto wadogo, za shule za msingi na  sekondari. Amependa kuulizia hata maswali wanafanya nini kwa siku nzima na kama walikuwa na furaha, kwa mujibu wa Mratibu wa “Kiangazi kwa vijana”, Padre Franco Fontana, ambaye ni  msimamizi wa Kikanisa cha Vikosi vya Ulinzi na Majumba ya Makumbusho. Kwa mshangao mkubwa vijana walibaki kimya kabisa na baadaye  walimzungusha kwenye Ukumbi na kuendelea na shughuli zao  za michezo ya kila siku.

Papa amejibu maswali yote kwa urahisi 

Hata hivyo Papa Francisko amependa iwe hivyo. Watoto watatu wamemuuliza maswali ambayo yalikuwa yamekwisha andaliwa kwani ndiyo ilikuwa nia ya  kumwandikia barua. Papa ameyajibu yote kwa urahisi tu na mwisho amesalimia na kuwashukuru watu 22 wanaowasaidia watoto na vijana hao. Kabla ya kuondoka wamepiga hata picha ya pamoja. Jambo ambalo limemshangaza Padre Franco ni kwa namna gani watoto wamempokea Papa kama kifamilia, urahisi na ubaba ambao wameishi kwa kipindi kifupi hicho.

Shughuli za michezo wakati wa kiangazi

Kituo hiki cha kiangaza kimefunguliwa kwa utashi wa Mamlaka ya Vatican ili kuwasaidia kidogo wazazi ambao wanafanya kazi Mjini Vatican. Kimefunguliwa mwezi huu wa Julai 2020 katika  shughuli za elimu, michezo na katika kutembelea  Bustani ndani ya Vatican. Shughuli za michezo zinafanyika katika Ukumbi wa Papa Paulo VI,  ambapo ni mamia ya watoto karibu ambao wanafika kia siku asubuhi, lakini pia kwa kufuata protokali za kuzuia maambukizi ya covid-19. Kituo kinaendeshwa na shirika la Mtakatifu Dono Bosco pamoja na chama kiitwacho “Yote ni siku kuu”. Kila siku shughuli pia ni katika bwawa la kuogelea, michezo ya mpira wa tenis, wa miguu na kikapu, na michezo mingine kama pic nic katika Bustan za Vatican.

21 July 2020, 09:07