2020.05.01 Misa ya Papa katika Kanisa la Mtakatifu Marta 2020.05.01 Misa ya Papa katika Kanisa la Mtakatifu Marta 

Mtakatifu Yosefu na Papa Francisko ni kama vile Papa Pio XII!

Papa Francisko ameadhimisha Misa katika siku ya Mei Mosi kwenye kikanisa cha Mtakatifu Marta Vatican akiwa karibu na sanamu ya Mtakatifu Yosefu mfanyakazi, huyo huyo ambaye alikuwa katika uwanja wa Mtakatifu Pietro na Papa Pacelli kunako mwaka 1956,mwaka mmoja baadaya ya kuitangaza kiliturujia kama siku kuu ya Mchumba wa Bikira Maria.

Na Sr. Angela Rwezaula –Vatican

Kama ilivyokuwa miaka 64 iliyopita, bila umati kwa sababu yetu  ya  siku za janga ,lakini na mlinzi huyo huyo wa wafanyakazi ambaye anatazama kikundi ambacho kimeguswa kwa namna ya pekee ya ugumu  wa kazi na mtazamo kwa wote, kama ilivyokuwa hata katika mkesha wa enzi za kijamii ambazo zilikuwa zinapaswa kuijenga kwa upya nchi ya Italia mara baada ya vita.

Sanamu kutoka Milano hadi Roma

Zaidi ya tofauti za kihistoria,kuna mambo yanayofanana sana juu ya sanamu ya Mtakatifu Joseph ambayo ililetwa mjini Vatican siku ya Alhamisi 30 Aprili  alasiri na kuwekwa katika kikanisa cha Mtakatifu Marta, kwa matazamio ya Misa iliyoadhimishwa katika asubuhi ya Mei Mosi, 2020 na Papa Francisko katika siku kuu ya Mtakatifu Yosefu. Na hii ilikuwa ni mwaka 1956 sanamu kama hiyo ilibarikiwa  kunako Mei Mosi  na aliyekuwa Askofu Mkuu wa Milano Giovanni Battista Montini  na kunako  Mei 2  ilisafirishwa na helikopta kuja Roma ili ibarikiwe pia na  Papa Pius XII  wakati wa Mkutano uliokuwa unafanyika siku hiyo na Chama cha wakristo wafanyakazi wa Italia (ACLI). Ni Mkutano ambao uliangukia miezi kumi na mbili baada ya Misa ambayo Papa Pacelli alikuwa ameifanya katika liturujia ya kuweka  wakfu sherehe ya Mchumba wa Maria na mlinzi wa Yesu kwenye sikukuu ya wafanyakazi ambayo  ilikuwa inaadhimishwa ulimwenguni kote .

Sanamu kuletwa mwaka 2015

Chama cha wakristo wafanyakazi wa Italia (ACLI) kama leo hii ambao wamependelea kulemtea Papa Francisko sanamu iliyotengenzwa kwa shaba na mchoraji Enrico Nell Breuning, ina  urefu wa sentimeta 150, iliyotunzwa katika makao makuu ya chama chao Roma. Kiukweli, sanamu hiyo ilikuwa tayari imewekwa mbali na Papa Francisko, wakati ilipoletwa katika  maandamano wakati wa Katekesi  katika Ukumbi wa Papa Paul VI kunako tarehe  23 Mei 2015.

Kazi iliyo huru na ya mshikamano

Mchezo wa marudio ambao unajumuisha mambo ya sasa, na wasiwasi mwingi unaotikisa ulimwengu wa kazi, kama vile wa zamani na  katika kumbu kumbu ya wale waliotutangulia na  ambapo, kwa mujibu wa maandishi ya Rais wa kitaifa wa  Chama cha Wakristo Wafanyakazi Italia, (ACLI ) Bwana Roberto Rossini, kwa Papa Ftancisko anasema : “inatutia moyo kufanya kazi ili kama ulivyo wewe Baba Mtakatifu ambaye  umesisitiza mara kwa mara kuwa, hakuna mfanyakazi ambaye hasiweze kuwa na haki na kazi iwe huru, ya ubunifu, shirikishi na ya mshikamano” "

01 May 2020, 10:45