Hospitali ya Regina Apostolorum  huko Albano Laziale Italia wamepokea msaada wa vifaa vya huduma kwa wagonjwa wa virusi vya corona kutoka kwa Papa Francisko. Hospitali ya Regina Apostolorum huko Albano Laziale Italia wamepokea msaada wa vifaa vya huduma kwa wagonjwa wa virusi vya corona kutoka kwa Papa Francisko. 

Vatican#coronavirus Papa atoa msaada wa vifaa muhimu vya kusaidia wagonjwa!

Hivi karibuni Papa Francisko ametoa msaada wa zana za kujikinga,barakoa na vifaa vingine muhimu ywa huduma kwa walioambukizwa na virusi katika Hospitali ya Regina Apostolorum la Shirika la Mabinti wa Mtakatifu Paulo.Ni kituo kilichogeuzwa kuwa cha Wagonjwa wa Covid-19.

VATICAN

Vioo vya kujikinga, barakoa na vifaa vingine muhimu vya lazima vya  msaada wa huduma kwa walioambukizwa vimeweza kufika katika Hospitali ya Regina Apostolorum la Shirika la Mabinti wa Mtakatifu Paulo huko Albano nchini Italia. Hivi karibuni nyumba hivyo imegeuzwa  kuwa Kituo cha Wagonjwa wa Covid-19.

Msaada huo umetolewa na Papa Francisko ambao umeelekezwa  kwa Askofu jimbo hilo  Askofu Marcello Semeraro. Katika vifaa hivyo vya huduma Papa Francisko ameidha ametuma kifaa kingine muhimu sana  cha kupumua kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa katika vyumba  vya mahututi katika kituo hicho hicho.

Kwa mujibu wa Papa Francisko amekusudia kuonesha ukaribu msaada huo kwa  wasimamizi wote, kwa wafanya kazi wote na  kwa namna ya pekee wale wote wenye maambukizi ya ugonjwa huo wa corona, ambapo Yeye binafsi  yuko karibu na kila mmoja wao kiroho kwa sala na kwa maana hiyo amewabariki kwa Baraka ya Kitume kutoka moyoni, kama msaada na nguvu kutoka mbinguni na faraja inayohitajika katika wakati huu.

Hayo yote yanasomwa kutoka katika Barua iliyotumwa kwa mwakilishi  wake wa  Sadaka ya Kitume  Kardinali Krejeweski. Kufuatia na tukio hili naye Askofu wa Jimbo Katoliki la Albano ametosa shukrani zake kwa Papa Francisko na kwa niaba ya uongozi wa Hospitali hiyo.

Shukrani pia zimemwendea Kardinali Konrad Krajewski, ambaye ni Msimamizi wa Sakadaka ya Kitume ambaye amemwakilisha  hivi karibuni Papa Francisko kuwafikishia msaada wa zana hizo muhimu katika wakati huu mgumu.

12 April 2020, 14:30