Gereza la wafungwa la Regina coeli lililoko katika moyo wa Roma Gereza la wafungwa la Regina coeli lililoko katika moyo wa Roma  

Uwakilishi wa Ofisi ya Katibu wa Vatican kutembelea wafungwa Regina Coeli

Katika Gereza la Regina Coeli jijini Roma kumefanyika maadhimisho ya misa kwa wafungwa.Wamekabidhi mshikamano uliokusanywa na watu wa Taasisi Vatican katika fursa ya siku za Majilio na Kuzaliwa kwa Bwana kwa ajili ya wenye shida pia Rosari zilizobarikiwa na Papa.

VATICAN

Jumapili asubuhi tarehe 2 Februari 2020 kikundi kutoka katika Ofisi ya Katibu wa Vatican kimetembelea Gereza  la wafungwa wa Regina Coeli jijini  Roma, ili  kushiriki maadhimisho ya Misa Takatifu ya Domiminika na kuwakabidhi zawadi za mshikamano uliokusanywa kutoka kwa wafanyazi wa Taasisi ya Vatican wakati wa kipindi cha Majilio na cha Kuzaliwa kwa Bwana kwa ajili ya watu wenye shida zaidi. Hayo yote yameelezwa na msemaji mkuu wa vyombo vya habari Vatican, Dk. Matteo Bruni.

Uhamasishaji wa kibinadamu

Baada ya maadhimisho ya misa  ambayo pia kulikuwapo na maombi ya waamini wafugwa pia  walikwenda kutembelea hata kituo kikuu cha Chama cha kujitolea kinachoongozwa na Mafrateli wafransiskani wakonventuali Vo.Re.Co,. Shughuli yao ikiwa katika kuhamasisha ubinadamu na ukristo kwa kuwasaidia wafungwa na wale wote ambao baada ya kutoka kifungoni wanatelekezwa na jamii.

Rosari zilizobarikiwa na Papa

Kabla ya kurudi Vatica, wawakilisho hao wameweza kukabidhi Padre msimamizi ya Kanisa dogo la magereza Vittorio Trani, rosari zilizo barikiwa na Papa Francisko ambazo alipokea wakati wa ziara yake nchini Thailand kwa lengo la kuwazawadia wenye shida.

03 February 2020, 11:05