Masikitiko ya Papa kwa waathirika wa ajali mbaya ya Bus nchini Burgaria
Na Sr. Angella Rwezaula - Vatican
Ajali ya Busi usiku ambalo liligeuka kuwa mtego wa moto kwa kusababisha vifo vya abiria 46 waliokuwa wamelala usingizi wakisafiri. Ni wanaume watatu, wanawake watatu na mvulana mmoja tu waliofanikiwa kuvunja madirisha na kujiokoa, lakini ambao hawatasahau tukio ambalo katika dakika chache lilibadilisha safari yao ya siku moja katika jiji la Istanbul ambapo walikuwa wameishi vizuri kabla ya ajali hiyo mbaya zaidi kutokea katika maisha kwenye barabara za Ulaya kwa miaka iliyopita.
Kufuatia na hilo hata Baba Mtakatifu Francisko amesikitishwa sana na habari hiyo, hasa kifo cha watoto 12 na kutuma, telegram yake iliyotiwa saini na Katibu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin, huku ikieleza mshikamano wa dhati na sala kwa waathirika na ukaribu kwa ajili ya manusura. Telegram hiyo imeelekezwa kwa rais wa Makedonia Kaskazini, nchi ambayo walikuwa wanatoka waathirika hao.
Tukio hilo la ajali lilitokea nchini Bulgaria, karibu na kijiji cha Bosnek. Moto wa Bus hilo ulilipuka mara baada ya gari la kampuni ya Beta Trans, maalum kwa ajili ya usafiri wa Istanbul, kuacha barabara. Wakati huo huo Makedonia imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa na kupeperusha bendera nusu mlingoti; hata nchini Bulgaria pia ilitangaza siku moja ya maombolezo na uchunguzi wa mamlaka ya Bulgaria kufunguliwa ili kutoa mwanga juu ya sababu za ajali, kuvunjika au makosa ya kibinadamu, ambayo yameharibu kabisa familia nyingi. Kwa maana hiyo watajaribu kuchunguza ikiwa safari hiyo ilifanywa kwa kufuata hatua na kanuni za usalama, pia kwa msingi wa shuhuda za walionusurika.