Mtandao wa Kimataifa wa nia za Sala umegeuka kuwa Mfuko wa Vatican
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.
Papa Francisko ameandika kwa maandishi yake kufuatia na uchaguzi binafsi kwa mujibu wa sheria ya Kanoni kuunda Mfuko wa Vatican ujulikanao “Mtandao Kimataifa wa Sala wa Papa”. Mtandao wa Kimataifa wa Sala ya Papa umekwisha kuwa tayari Utume wa Sala, ulionzishwa nchini Ufaransa na Padre François-Xavier Gautrelet, S.J., na ambao unasimika mzizi yake juu ya Roho ya Moyo Mtakatifu wa Yesu na kupokea nia za kila mwezi za sala, zinazopendekezwa na Baba Mtakatifu. Katika kuundwa huko, shirika hilo la kijesuit ndilo litawajibika kushughulikia utume huo.
Katika maelezo yake amesema “Miaka kadhaa iliyopita, Papa Francisko anaandika kuwa, niliridhia Mtandao wa Kimataifa wa Nia ya Maombi ya sala ya Papa kama Shughuli ya Kipapa kwa ajili ya kusisitizia tabia ya ulimwengu kwa ajili utume huo na ulazima ambao watu wote wanapaswa kusali daima na zaidi kwa moyo wa dhati. Kwa lengo la kuratibu na kuweka chachu ya harakati hii ya kiroho na ambayo Papa ameseme anapendezwa nayo na kwa maana hiyo ni , kuipa muundo unaostahili wa kipindi tunachoishi, kwa kuzingatia ukuu wake wa kitume katika Kanisa na kwa ajili ya ukuu wa Serikali ya ya mji wa Vatican.
Katika muktadha wa sheria Kanoni na kifungu cha 1 n. 1 ya Sheria Msingi ya Mji wa Vatican ya tarehe 26 Novemba 2000 na kwa kukubali ombi lililowasilishwa na Mtandao wa Maombi Ulimwenguni wa Papa, ameridhia yeye binafsi sheria ya kanoni na Mfuko wa Vatican “wa Mtandao wa Sala ya Papa” kwa kuwa na Makao yake katika Mji wa Vatican, inayosimamiwa na Sheria zilizounganishwa na Maandishi(Chirograph)haya, iliyoidhinishwa na mimi leo, na ambayo itaanza kutumika kuanzia tarehe 17 Desemba 2020. Barua hiyo imetiwa saini Mji wa Vatican, tarehe 17 Novemba 2020.