Papa akumbusha siku ya Mtakatifu Yohane Paulo II na utume wa mkristo ni sala!
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Mara baada ya Katekesi, Jumatano tarehe 21 Okotb 2020, Papa Francisko amewasalimia mahujaji na waamini kwa lugha mbali mbali, na amekumbusha mwezi wa kimisionari na kusisitizia wito kwa wakristo wote kuhisi uwajibikaji katika kutangaza na kueneza Ufalme wa Mungu na kama ilivyo hata umuhimu wa sala kwa ajili ya ubinadamu, hasa kwa maskini na kwamba utumewa kwanza wa kimisionari ni sala.
Mtakatifu Yohane Paulo II alikwa na ibada ya kina
Akiwageukia mahujaji na waamini wa lugha ya kipoland amewakumbusha juu ya Mama Kanisa katika lirurjia ya tarehe 22 Oktoba inakumbuka Siku ya Mtakatifu Yohane Paulo II ambayo inaangukia katika mwaka wa Jubilei ya miaka 100 tangu kuzaliwa kwake. Yeye alikuwa mtu wa kiroho kwa kina, kila siku alikuwa akitafakari uso angavu wa Mungu katika liturujia ya sala na tafakari ya zaburi. Alikuwa akiwashauri wakristo wote kuanza na siku kwa kusifu Bwana kabla ya kuanza shughuli zozote ambazo daima siyo rahisi katika maisha ya kila siku na hivyo amewabariki.
Sala inafungua mlango wa maisha kwa Mungu
Kwa waamini wa lugha ya kireno, Papa Francisko ameakumbusha juu ya sala inavyo fungua mlango wa maisha yao kwa Mungu. Na kwamba Mungu anafundisha namna ya kutoka nje yao binafsi ili kwenda kukutana na wale walioko kwenye majaribu, kwa kuwapatia wao faraja, matumaini na msaada. Kwa moyo wote awabariki na baraka ya Mungu.