Mkutano wa Familia Duniani Dublin 21 -26 Agosti 2108 Mkutano wa Familia Duniani Dublin 21 -26 Agosti 2108 

Papa awakumbusha Ireland kuwaandalia vijana wakati endelevu!

Katika tazamio la Ziara ya Kitume huko Ireland, Siku ya Jumamosi na Jumapili ya wiki hii, kwenye Mkutano wa IX wa Familia Duniani, Baba Mtakatifu Francisko ametuma ujumbe kwa njia ya wake akikimbusha umuhimu wa kuandalia vijana wakati endelevu

Sr.Angela Rwezaula - Vatican 

Rafiki wapendwa, nikiwa najiandaa kwa siku za hivi karibuni kutembelea Ireland, kwa ajili ya Mkutano wa Familia duniani, ninapenda kuwatumia salam za upendo watu wote wa Ireland: Ninafurahi ninapofikiria ninarudi Ireland!

Hayo ndiyo maneno ya mwanzo wa ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko alioutuma kwa njia ya Video Jumatatu 20 Agosti jioni kwa watu wote wa Ireland katika matazamio  zira yake ya kitume kwenye Mkutano wa IX wa Familia Duniani, ziara ambayo ni ya siku mbili kuanzia tarehe  25-26 Agosti, na hivyo katika ujumbe huu anakumbusha umuhimu wa kuandalia vijana wakati endelevu.

Katika ujumbe wake anasema  “Kama mnavyojua kuwa Mkutano wa dunia ni maadhimisho ya uzuri wa mpango wa Mungu kwa ajili ya familia; lakini pia ni fursa kwa ajili ya familia kutoka pande zote za dunia kukutana na kusaidiana kwa pamoja katika kuishi wito wao maalum. Famili leo hii inakabiliana na changamoto nyingi katika juhudi zao, ili kujikita katika upendo mwaminifu, kuwalea watoto katika thamani iliyo safi na ili wawe jumuiya kubwa, chachu ya wema, upendo na kutunzana kwa pamoja. Ninyi mnatambua hili.

Kadhalika Baba Mtakatifu anaendelea “ Ni matumaini ya kuwa fursa hiyo inaweza kuwa kisima cha upyaisho wa kutia moyo familia za kila pande ya dunia na  hasa familia zile ambazo zitaweza kuwapo huko Dublin. Wanaweza kukumbuka nafasi msingi ya familia katika maisha ya jamii na katika ujenzi wa wakati endelevu ulio bora kwa vijana. Kwani vijana ni wakati endelevu! Ni muhimu sana kuwaandaa vijana kwa ajili ya wakati endelevu,kwa maana ya  kuwaandalia leo hii, kwa wakati uliopo, lakini pia kwa njia ya mizizi ya wakati uliopita: ikiwa na  maana ya vijana na babu zao: Ni muhimu”.

Kama ilivyo sababu maalumu ya ziara yangu kutembelea Ireland ni kuhusu Mkutano wa Familia duniani, lakini ninapendelea  iwe kama fursa ya kuwakumbatia familia nzima ya Ireland. Ninasali kwa namna ya pekee  ili mkutano uweze kusaidia kukua kwa umoja na mapatano kati ya waamini wote wa Kristo, kama ishala ya amani ya kudumu ambayo ni ndoto ya Mungu kwa ajili ya familia nzima ya binadamu.

Ninatambua jinsi gani kwa ari zote  watu wanajitahidi kuandaa ziara yangu. Shukrani zangu za dhati kwa wote. Ninaomba kwa kila mmoja asali ili mkutano huo uweze kuwa kipindi cha furaha na hata cha utulivu, chenye kuwa na upendo mtulivu  wa Yesu kwa familia zote na ukweli kwa ajili ya kila mtoto wa Mungu. Ninawakikishia ukaribu wangu, sala zangu na kuwaalika kusali kwa ajili yangu kwa maana ninahitaji. Na kwa moyo wote ninawabariki.

Mungu awabariki. Kwa jina la Baba, na la Mwana , na  Roho Mtakatifu. 

 

22 August 2018, 12:56