Tunaweza kumkiri Yesu kuwa ni Bwana kwa neema ya Roho Mtakatifu Tunaweza kumkiri Yesu kuwa ni Bwana kwa neema ya Roho Mtakatifu 

Kumkiri Yesu kuwa ni Bwana ni neema ya Roho Mtakatifu

Ikiwa hatukubali njia ya Yesu,njia ya unyenyekevu aliochagua Yeye kwa ajili ya wokovu,si kwamba sisi siyo wakristo tu,bali tanastahili kuitwa kile ambacho Yesu alimwambia Petro “Nenda nyuma yangu shetani!” Ni katika tafakari ya Papa Francisko tarehe 20 Februari 2020 wakati katika Kanisa la Mtakatifu Marta Vatican.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Watu wanasema mimi ni nini? Je ninyi mnasema mimi ni nani? Ni maswali yaliyomo katika Injili ya Liturujia ya siku  ya Alhamisi 20 Februari 2020 ambayo Papa Francisko ameanza nayo katika tafakari yake kwenya Kanisa la Mtakatifu Marta, Vatican. Papa amesema Injili inatufundisha kunia zile  nyayo ambazo mitume tayari walipitia ili kuweza kumtambua Yesu ni nani. Nazo ni tatu, kumjua, kumkiri na kukubali njia ambayo Mungu amechagua kwa ajili Yake.

Kukiri Yesu kwa neema ya Roho Mtakatifu

Kumjua Yesu ni tendo ambalo  tunafanya sisi wakati tunaposhika Injili mikononi mwetu na kujaribu kumjua Yesu; tunapo wapeleka watoto katika katekisimu (…); tunapowaleka kuudhuria Misa, lakini hiyo ni hatua moja tu, anambainisha Papa, na hatua ya pili ni ile ya kuungama kwa Yesu.  Lakini kufanya hivyo peke yetu hatuwezi. Katika Injili ya Matayo Yesu alimwambia Petro “hayo hayakutokana na wewe. Ni Baba yangu aliyekujalia” . Tunaweza kukiri Yesu tu kwa njia ya nguvu ya Mungu na kwa njia ya Roho Mtakatifu. Hakuna yeyote awezaye kusema Yesu ni Bwana bila kuwa na Roho. Kwa maana hiyo Jumuiya ya kikristo inatakiwa daima kutafuta nguvu ya Roho Mtakatifu ili kukiri Yesu na kusema kuwa Yeye ni Mungu  na kwamba Yeye ni Mwana wa Mungu.

Kukubali njia ya Yesu hadi msalabani

Lengo la maisha ya Yesu nini?  Kwa nini alikuja? Papa anatoa maswali haya  na kujibu. Kujibu swali hili maana yake ni kutimiza hatua ya tatu ya kumtambua Yeye. Papa Francisko amekumbusha kuwa, Yesu alianza kufundisha mitume kwamba, ilitakiwa ateseke, auawe na baadaye afufuke. Kukiri Yesu ni kuthibitisha kifo na ufufuko wake; siyo kukiri kuwa wewe ni Mungu na kusimama hapo, hapana! “ ni kusema kuwa wewe umekuja kwa ajili yetu na umekufa kwa ajili yangu. Wewe umefufuka. Wewe unatupatia maisha, Wewe umetoa ahadi ya Roho Mtakatifu wa kutuongoza”.

Kukiri Yesu maana yake ni kukubali njia ambayo Baba amechagua kwa ajili yake yaani unyenyekevu. Barua ya Paulo kwa Wafilipi anasema: “ Mungu alimtuma Mwanae akajikana na  akawa mtumishi, akanyenyekea hadi mauti, mauti ya msalaba”. Ikiwa hatukubali njia ya Yesu, njia ya unyenyekevu alioichangua Yeye kwa ajili ya wokovu, si kwamba si wakristo tu, bali tunastahili kile ambacho Yesu alimwambia Petro:“ Nenda nyuma yangu shetani!”

Asiyefuata njia ya unyenyekevu siyo mkristo

Papa Francisko katika ufafanuzi wake wa Injili ya Siku amebainisha pia suala la  Shetani kuwa anajua vema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, lakini Yesu anakataa kikiri kwake kama alivyo mwondoa hata Petro aliyekuwa anakataa njia aliyochagua Yesu. Kukiri Yesu ni kukubali njia ya unyenyekevu na kunyenyekeshwa. Ikiwa Kanisa halitembei katika njia hiyo ni kukokosea na kugeuka ya kidunia. Ikiwa tunaona wakristo wengi wema, wakiwa na mapenzi mema, lakini ambao wanachanganya dini na dhana ya wema wa kijamii, wa urafiki na wakati tukiona makleri wengine ambao wanasema wanafuata Yesu, lakini wanatafuta sifa, njia zenye mikato na sikikuu, njia za kidunia, jua wazi kwamba hawatafuti Yesu bali ni kujitafuta wao binafsi.

Uthabiti wa kikristo katika maisha na katika huduma

Siyo wakristo ambao wanasema ni wakristo lakini kwa jina tu, kwa sababu hawakubaliani na njia za Yesu, za unyenyekevu.  Tunasoma  hata katika historia ya Kanisa, Papa Francisko anasema kwamba maaskofu wengi waliishi namna hii na hata mapapa wa kidunia ambao  hawakujua njia ya unyenyekevu; hawakukubaliana nayo, kwa maana hiyo Papa Francisko anahimiza kuwa “lazima kujifunza kuwa ile haikuwa ni njia”.  Papa Francisko amehitimisha akiomba neema ya kuwa na uthabiti wa kikristo katika huduma za maisha  na  neema ya njia yake ya unyenyekevu na isije kuwa ile ya ukristo wa kubabaisha.

 

20 February 2020, 14:47
Soma yote >