Nyumba za Familia nyingi za Kipalestina huko Gaza zimeharibiwa Nyumba za Familia nyingi za Kipalestina huko Gaza zimeharibiwa 

Nchi Takatifu:Sadaka ya Jumapili 30 Mei kwa ajili ya jumuiya za Gaza

Jumapili tarehe 30 Mei,katika siku kuu ya Utatu Mtakatifu,Patriaki wa Yerusalemu, amewaomba waamini wote wa upatriaki kutoa mchango wao kwa ajili ya kusaidia waamini wengi wa Jumuiya za kikristo huko Gaza ambao wamejikuta katika ghasia na mashambulizi yaliyotokea hivi karibuni na kuwaacha na madhara mwakubwa mno.Uharibifu wa nyumba na miundo mbinu.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Patriaki wa Yerusalemu, Askofu Mkuu Pierbattista Pizzaballa ameomba Parokia zote na makanisa ya majimbo kutoa mchao wao wakati wa sadaka ya Jumapili tarehe 30 Mei ambapo Mama Kanisa anaadhimisha Siku Kuu ya Utatu Mtakatifu, kwa ajili ya Jumuiya za Gaza na mahitaji yao yaliyojitokeza katika ghasia za  hivi karibuni

Katika barua yake iliyochapishwa kwenye Wavuti wa Upatriaki, Askofu Mkuu Pizzaballa amewaalika waamini wote kuwa na moyo mwema na mtazamo kwa ajili ya watu wenye kuhitaji zaidi hasa kwa ajili ya Gaza mahalia mbapo wao wamepata madhara makubwa ya mabomu kwa siku za hivi karibuni.

Mateso ya Gaza yamezidi kuongezeka katika ghasia na mashambilizi hayo kwa wakazi wa Gaza, wakati huo huo wakiendelea na mapambano dhidi ya Covid- 19 amesisitiza Patriaki. Kwa maana hiyo kiongozo huyo wa Upatriaki ameomba kwa moyo wote waweze kuchangia ili kutoa faraja katika mateso ya ndugu hao waamini wakristo. Na Mpango huo unataka kuwa ishara ya mshikamano kutoka majimbo yote ya upatriaki wa kilatino.

26 May 2021, 15:36