Kuwaachilia huru watawa waliokuwa wametekwa nyara nchini Haiti
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Watawa wa 4 wa mwisho wamewachiliwa huru waliokuwa wametekwa nyara mnamo Aprili 11 huko Haiti. Ni tukio ambalo limefanyika usiku kati ya Alhamisi 29 na 30 Ijumaa Aprili. Habari hiyo, ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa muda, imetolewa na makuhani wa Shirika la Mtakatifu Jacques ambao kati ya wengine wanatoka shirika hilo. Ni wiki moja tu iliyopita, watekwaji nyara wengine watatu walikuwa wameachiliwa huru.
Kumshukuru Mungu
Mmoja wa watawa hao amethibitisha kuwa na afya njema na kuwashukuru mabalozi wa Ufaransa na Marekani kwa juhudi zao katika kusuluhisha jambo hilo, lakini pia na viongozi wa eneo hilo kwa msaada wao . “Maneno yetu ya kwanza yana waendea kaka na dada zetu walioachiliwa huru, kuwaonesha furaha yetu na kuridhika kwetu kwa kuwakuta salama salimini”. Kwa kuongezea, “tunazo hisia za shukrani kubwa kwa Mungu na kwa watu wote na taasisi ambazo zimehusika kufikia ukombozi wa ndugu zetu na marafiki zetu, ambao tumepamban mwili na roho”. Kikundi cha watu 10 kilisimamishwa huko Croix-des-Bouquets, karibu na mji mkuu Port-au-Prince wakati wakielekea parokia ya Galette Chambon, huko Ganthier, kushiriki sherehe za kusimikwa kwa kasisi wa parokia, Padre Jean Arnel Joseph, inayoundwa na makuhani watano Wakatoliki, watawa wa kike wawili na walei watatu. Kwa upande wao walikuwa wameomba fidia ya dola milioni.
Ukosefu wa usalama Haiti
Utekaji nyara umeathiri na kuleta mkanganiko sana wa maoni ya umma na umebainisha wazi ukosefu mkubwa wa usalama ambao Haiti inaishi kwa sasa, nchi ambayo baada ya tetemeko la ardhi lenye uharibifu wa miaka 11 iliyopita, haijapata furaha kwa sababu ilikumbwa na majanga ya asili na shida za kijamii, kiuchumi na kisiasa ambazo sasa zimepelekea vurugu za magenge yenye silaha. Katika taarifa iliyosainiwa wiki chache zilizopita na askofu mkuu wa mji mkuu, Askofu Max Leroy Mésidor, alikuwa analaani kushuka kwa maadilini ya kijamii ya wahaiti.