03.10.2020:Sudan na vikundi vikubwa vya waasi vinasaini makubaliano ya amani huko Juba 03.10.2020:Sudan na vikundi vikubwa vya waasi vinasaini makubaliano ya amani huko Juba 

Sudan:Wcc amesema mkataba wa amani nchini Sudan ni tumaini jipya kwa raia!

Kufuatia na kutiwa saini ya makubaliano ya amani nchini Sudan na vikundi vikubwa vya waasi huko Juba tarehe 3 Oktoba,makanisa nchini humo wanasema huo ni upeo mpya wa amatumaini ya amani ya kudumu kwani watu wamechoka sana na vita.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Makanisa ya Kikristo (Wcc)nchini Sudan wanatazama kwa mapya ya amani  ya kudumu katika makubaliano yaliyotiwa saini mnamo Oktoba 3 huko Juba na wawakilishi wa serikali ya mpito na vikundi vikuu vya waasi wa nchi hiyo na upatanishi wa Sudan Kusini. Kwa mujibu wa Mchungaji William Deng Mian,Katibu mkuu wa Baraza la Mkanisa nchini Sudan (Nccs) ameelezea furaha yake na kwamba watu kweli wamechoka na vita na wanataka amani. Kila jitihada ambayo inasaidia kusimamzisha silaha na kuruhusu watu waishi kwa amani inakaribishwa kwa moyo mweupe, kwa mujibu wa nchungaji huyo wa Wcc.

Makubaliano hayo yanafuta mkataba wa kwanza wa pamoja uliotiwa saini mnamo tarehe 31 Agosti  mwaka huu na ulisainiwa na Chama cha Mapinduzi cha Sudan(SRF), kinachojumuisha waasi kutoka Darfur, kusini mwa Kordofan na Blue Nile, mikoa mitatu ambayo waasi wa Sudan wamepambana kwa umwagaji damu dhidi ya ubaguzi uliofanywa na Khartoum wakati wa urais wa mkuu wa zamani wa nchi, Omar al-Bashir. Makubaliano hayo yanashughulikia masuala kadhaa muhimu: usalama; kugawana madaraka, fidia, kurudi kwa wakimbizi wa ndani  na wakimbizi, udhibiti wa ardhi ambazo kiutamaduni zinatumiwa na jumuiya za kikabila na ujumuishaji wa wanamgambo waasi katika jeshi la kawaida la Sudan.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu nchini Sudan  Kusini na Sudan Scbc) Padre Musa Timothy ameonesha furaha yake ya kufikia hitimsho hili lilioanza mwaka mmoja uliopita “ Makubaliano ya amani yanapokelewa na kupongezwa na watu wote wa  Sudan kwa ujumla lakini pia hasa kwa watu wa Darfur, kwa sababu ni kuhitmishwa kwa vita na mateso yaliyoanza tangu mwaka 2003 amesisitiza Padre huyo.

12 October 2020, 16:05