Papa Francisko:Misale Mpya ya CEI itaanza kutumika rasmi wakati wa Pasaka 4 Aprili 2021!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Aina mpya ya dhati ya zamani ambayo ina mizizi yake kutoka katika Mtaguso wa II wa Vatican, ndiyo Misale mpya ya Baraza la Maaskofu Italia (CEI) ambayo Papa ameifungua mikononi mwake asubuhi, tarehe 28 Agosti 2020, akiwa amezungukwa na Kardinali Gualtiero Bassetti, rais wa Baraza la maaskofu Italia na kikundi kilichofanya kazi ya kuandaa misale hiyo na ambapo Papa alipendelea kuitambua kazi hiyo na kuwashukuru ujio wao.
Kurasa za utamaduni hai
Papa Francisko ameshukuru zawadi aliyoipokea kwa kusisitiza umuhimu wa kazi iliyofanyika na mwendelezo wa Mtaguso wa Pili wa Vatican, kwa mujibu wa taarifa kutoka Baraza la Maaskofu Italia. Katika maneno ya Kardinali Bassetti anabainisha kwamba, Kitabu cha Misale ya waamini siyo zana ya kiliturujia tu, bali ni marejeo na sheria ambazo zinahifadhi utajiri wa utumaduni hai wa Kanisa na kukabidhiwa kwake kunageuka kwa mara nyingine tena kuwa fursa ya thamani ya mafunzo kwa wabatizwa wote.
Lugha imesasishwa na tarehe rasimi ni 4 Aprili 2021
Kitabu ambacho maparokia wataanza kutumia mara moja, lakini lakini rasimi ni kuanzia Dominika ya Pasaka ya tarehe 4 Aprili 2021 kimeridhiwa kwa mujibu wa makubaliano na Baraza la Maaskofu na kukubaliwa na Papa Francisko tangu tarehe 16 Mei 2019. Mbali na tofauti na uboreshaji wa toleo la tatu la Kilatino, misale hii inapendekeza maandishi mengine ya hiari ya muundo mpya, yenye kujibu zaidi hali hali halisi ya lugha na kiuchungaji katika jumuiya, na kwa kiasi kikubwa tayari inatumiwa tangu toleo la pili nchini Italia la mwaka 1983 .
Habari mpya: mabadiliko ya sala ya baba yetu na utukufu
Miongoni mwa taarifa mpya, ambayo tayari unajulikana, ni kwamba kutakuwa na mabadiliko kuhusu sala ya Baba Yetu katika sehemu isemayo ‘usitutie katika kishawishi’ na badala yale inakuwa usituache katika kishawishi, na wakati katika utukufu mahali isemwapp ‘amani duniani kwa watu wenye mapenzi mema’ inabadilishwa na usemi kuwa amani duniani kwa watu, waliopendwa na Bwana. Misale hiyo ni ya kwanza kuchapishwa na Mfuko wa Jumuiya wa Dini ya Watakatifu Francis wa Assisi na Catherina wa Siena katika muundo mmoja na itasambazwa na Duka la Vitabu Vatican kuanzia mwishoni mwa mwezi Septemba.