Tafuta

2023.05.14 Sala kwa ajili ya amani nchini Ukraine kwa sababu vita bado vinaendelea kwa kasi. 2023.05.14 Sala kwa ajili ya amani nchini Ukraine kwa sababu vita bado vinaendelea kwa kasi. 

Ukraine:milipuko yenye nguvu usiku huko Kyiv&Ziara ya Zelensky Ulaya imehitimishwa!

Mashambulizi makali ya Urussi uwanjani yanaendelea.umla ya makombora 18 ya anga,bahari ni na ardhini yalirushwa dhidi ya nchi.Kwa mujibu wa Valeriy Zaluzhny,kamanda mkuu wa vikosi vya jeshi la Ukraine,Makombora yote yaliharibiwa na vikosi na njia za ulinzi wa anga cha Kikosi cha Wanajeshi wa Anga cha Ukraine.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Karibu milipuko kumi yenye nguvu ilisikika usiku wa tarehe 15 Mei huko Kyiv. Kengele za hatari ya  mashambulizi ya anga inafanya kazi katika mikoa yote ya nchi, kutokana na mashambulizi ya Kirussi ya kiwango cha kipekee, na idadi kubwa ya makombora katika muda mfupi zaidi: utawala wa kijeshi wa mji mkuu wa Kiukreine umetangaza jambo hilo. Meya wa Kyiv Vitaliy Klitschko alisema vifusi vya roketi hizo vimeanguka katika wilaya mbalimbali, huku jengo moja likiharibiwa huko Solomyanskyi magharibi mwa Kyiv. Kuna watatu waliojeruhiwa kufuatia uvamizi wa Urussi uliofanywa usiku.

Makombora yamelipuka huko Kyiv nchini  Ukraine usiku wa kuamkia tarehe 16 Mei 2023
Makombora yamelipuka huko Kyiv nchini Ukraine usiku wa kuamkia tarehe 16 Mei 2023

Wakati huo huo, Rais wa Ukraine Volodymir Zelensky alihitimisha safari yake barani Ulaya. Kutoka kwa ndege iliyokuwa ikimpeleka nyumbani, alielezea kufurahishwa kwake na mkutano na Papa Francisko na kwa msaada uliothibitishwa na Italia, Ujerumani, Ufaransa na Uingereza. “Kuna uungwaji mkono zaidi wa kujiunga kwetu na Umoja wa Ulaya, kuelewa zaidi kwamba uanachama wa NATO wa Ukraine hauwezi kuepukika,” alisema, akithibitisha kwamba silaha hizo mpya zitatumika kupinga Urussi na mashambulizi mapya ya kukabiliana nayo. Kituo cha mwisho kilikuwa  jijini London, ambapo rais wa Ukraine alipata ahadi kutoka kwa Waziri Mkuu wa Uingereza Sunak kusambaza mamia ya makombora mengine ya ulinzi wa anga na ndege mpya za masafa marefu zaidi ya kilomita 200.

Majeruhi ya  raia

Mashambulizi ya roketi yanaonekana kuongezeka pande zote mbili za mstari wa mbele nchini Ukraine, kulingana na Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu. Tangu tarehe 24 Februari 2022, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Masuala ya Kibinadamu Martin Griffiths alisema, kumekuwa na waathrika  wa kiraia 23,600 wa Ukraine, lakini inahofiwa kwamba idadi halisi itakuwa kubwa zaidi. Bwana Griffiths alisisitiza kwamba changamoto kubwa inahusiana na kushinda vikwazo vya kufikia maeneo yote ya Donetsk, Luhansk, Kherson na Zaporizhzhia, ambayo kwa sasa iko chini ya udhibiti wa kijeshi wa Urussi, na ni lazima kuchunguza chaguzi zote ili kufikia raia, popote walipo.

Rais wa Ukraine alikutana Waziri Mkuu wa Italia
Rais wa Ukraine alikutana Waziri Mkuu wa Italia

Kwa hiyo katika zira ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alitua London kwa mshangao asubuhi tarehe 15  Mei, kama sehemu ya ziara yake ya Ulaya ambayo ilimshuhudia akisimama Italia,  mjini Vatican, Ujerumani na Ufaransa. Katika mji mkuu wa Uingereza, Bwana Zelensky aliwasili kwa helikopta ya kijeshi huko Checkers, makazi ya Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak, ambaye alimkaribisha kwa kusema: “Ujasiri na ujasiri wa Rais Zelensky na Ukraine ni msukumo kwa sisi sote.” Na kwa upande wa kiongozi wa Kiukraine alitoa shukrani za dhati  kwa msaada mkubwa wa kijeshi uliotolewa na London kwa Kyiv. Hakika, London itathibitisha usambazaji zaidi wa mamia ya makombora ya ulinzi wa anga na mifumo ya angani isiyo na rubani, ikijumuisha ndege mpya zisizo na rubani za masafa marefu zenye safu ya zaidi ya kilomita 200. Nyenzo ambazo zitawasilishwa katika miezi ijayo  nchini Ukraine inapojiandaa kuongeza upinzani wake kwa uvamizi unaoendelea wa Urussi. Na Waziri Mkuu wa Uingereza alitoa wito kwa washirika wa Magharibi kutoa msaada wa kijeshi wa Kyiv katika wakati huu muhimu katika upinzani wa Ukraine kwa vita vya kutisha vya uchokozi ambavyo haikuchagua au kuchochea”.

tarehe 13 Mei 2023 Baba Mtakatifu akukutana na Rais wa Ukraine
tarehe 13 Mei 2023 Baba Mtakatifu akukutana na Rais wa Ukraine

Na wakati huo huo Bwana Zelensky Dominika tarehe 14 Mei 2023  alikuwa Paris,  Ufaransa, ambapo alikaribishwa na Rais Emmanuel Macron na kufanya mazungumzo na viongozi wa Ufaransa. Wakati wa chakula cha jioni Bwana Zelensky aliomba kama alivyofanya hata  jijini  Roma na Berlin, Ujerumani  silaha za kisasa zaidi kama vile  mizinga, jeti, na silaha za kupambana na ndege. Kiongozi huyo pia alithibitishwa na washirika hao watatu wa Ulaya, wakisisitiza kwamba msaada unahitajika ili kuanzisha mashambulizi ya kukabiliana na machafuko na kupata ushindi wa mwisho. Ni hapo tu, alisema, kutakuwa na msingi wa kuanza mazungumzo na Moscow. Rais wa Ufaransa Macron na mwenzake wa Ukraine pia wametoa wito wa kuwekewa vikwazo vipya dhidi ya Urussi kufuatia mkutano wao wa kilele wa pande mbili mjini Paris.

Makombora nchini Ukraine
16 May 2023, 13:49