Ziara ya Papa Francisko nchini Iraq ni ishara ya matumaini,unesco
Na Sr. Angela Rwezaula-Vatican.
Tangu Papa Francisko kuanza ziara yake ya kitume nchini Iraq kwa siku tatu hadi tarehe 8 Machi, imepata maoni mengi na mitazamo mbali mbali kutoka sekta mbali mbali, wakuu wa mataifa na mashirika. Kwa mfano Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO kufuatia na ziara hiyo linasema ni ishara ya matumaini na fursa ya kuimarisha jitihada za amani, na umoja nchini humo.
UNESCO kupitia taarifa yake imesisitiza “ziara ya Papa Francisko inakuja na ujumbe wa amani na umoja ikiungwa mkono na utofauti wa wairaq. Ujumbe huu uko katika mamlaka yetu kuu ya kuelewana, kuheshimiana na hatimaye kuwa na dunia yenye amani na haki.” Papa Francisko aliwasili Iraq siku ya Ijumaa tarehe 5 Machi ambapo Jumamozi alikwenda mji wa kaskazini huko Mosul na mabpo siku ya Jumapili tarehe 7 Machi amesali na waathirika wa mzozo unaliosababishwa na magaidi wa ISIL na uliosababaisha maelfu na maelfu ya watu. Kwa mujibu wa UNESCO inasema “Ziara ya Mosul inabeba ujumbe muhimu, mji ambao ni wa kale zaidi duniani na kituo cha kitamaduni na kidini, mji ambao umekumbwa na uharibifu mkubwa tangu magaidi wa ISIL wadhibiti mji huo kati yam waka 2014 hadi 2017”.
Jumuiya za Kikristo Iraq zimetambua mateso na ushahidi: Kwa wastani jumuiya za Kikristo za Iraq zimetambua na kujua miaka ya kuuawa kishahidi kwa sababu ya vita na mateso, ambayo yamesukuma mamia ya maelfu ya Wairaq kuondoka katika nchi yao. Sasa, inaonekana ni nafasi ya kugeweza kugeuza ukurasa na kuchangia ujenzi wa jamii nzima. Ni mwanzo ambao siyo rahisi ambao unahitahi nguvu na umakini wa kimataifa Jitihada na msaada uliotolewa na mashirika ya Kanisa ya kimisaada kwa mujibu wa Bwana Alessandro Monteduro, mkurugenzi wa tawi shirika la Misaada la Italia kwa upande wa Shirika la Kipapa la Kanisa hitaji ansema zimekuwa msingi wa kuruhusu jamii za Kikristo kuishi, hasa kaskazini mwa Iraq.
Jitihada za kifedha na shirika ambalo linatpekea kwenye kambi za mapokezi limepelekea familia zote za Kikristo zilizobaki kurudi kwenye nyumba za kweli. Bwana Monteduro ameongeza kusema kuwa: “Leo tunaweza kuwasalimia kwa furaha ukweli kwamba asilimia 45% ya Wakristo ya wale elfu 120,000 ambao walilazimika kukimbia mnamo 2014 wamerudi katika vijiji vya Bonde la Ninawi, kwa namna hiyo sehemu pendwa ya utuamaduni wetu”.