Lishe nchini India katika kipindi cha Janga la COVID-19 Lishe nchini India katika kipindi cha Janga la COVID-19 

Ripoti mpya ya Unicef,Fao,Wfp na Who kuhusu lishe Asia na Pasifiki

Katika eneo lenye watu wengi ulimwengi linahitaji kuongeza juhudi ya kuhakikisha lishe bora kwa watu waatao bilioni mbili barani Asia na Pasifiki kutokana na muktadha wa janga la Covid-19.Ni kwa mujibu wa Ripoti ya Mashirika ya umoja wa Mataifa ya INICEF,FAO,WFP na WHO.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotangazwa leo na UNICEF, FAO, WFP WHO, kuhusu muktadha wa kiuchumi uliosababaishwa na COVID-19 juu ya eneo lenye watu wengi ulimwenguni linahitaji kuongeza juhudi ili kuhakikisha lishe bora na lishe kwa watu wapatao bilioni 2 huko Asia na Pasifiki ambao hawakuweza kufuata lishe bora hata kabla ya janga hilo kutokea. Kwa mijibu wa ripoti iliyopewa jina: “Ripoti ya Asia na Pasifiki ya Usalama wa Chakula na Lishe 2020: Mlo wa Mama na Mtoto katika Moyo wa Kuboresha Lishe” iliyozinduliwa huko Bangkok inaonesha kuwa watu bilioni 1.9 walikuwa hawali lishe bora, hata kabla ya janga la COVID-19.

Kwa sababu ya bei ya juu ya matunda, mboga mboga na bidhaa za maziwa, imekuwa vigumu kula chakula bora kwa watu maskini katika Asia na Pasifiki. Ufikiaji nafuu wa lishe bora ni muhimu kuhakikisha usalama wa chakula na lishe kwa wote kwa akina mama na watoto hasa. Bei ya chakula na mapato yanayoweza kutolewa huhamisha maamuzi ya familia juu ya ulaji wa chakula na lishe. Lakini janga la COVID-19 na ukosefu wa nafasi nzuri za kazi katika maeneo mengi ya mkoa, pamoja na kutokuwa na uhakika mkubwa katika mfumo wa chakula na masoko, imesababisha kuzidi kutokuwepo kwa usawa, kwani kaya masikini zilizo na kipato kidogo zinabadilika. lishe yao kwa kuchagua vyakula vya bei rahisi na visivyo na lishe.

Nchini India imeanza kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni kubwa zaidi duniani ya utoaji chanjo dhidi ya virusi vya corona au COVID-19, ikipeleka maelfu kwa maelfu ya wahudumu wa afya wenye ujuzi na kwa msaada wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO. Kwa mujibu wa duru za Habari takriban wahudumu wa afya milioni 10 wanalengwa kuchanjwa katika duru ya kwanza ya kampeni hiyo, wakifuatiwa na wahudumu wengine walio msitari wa mbele kama vile polisi, vikosi vya ulinzi na wafanyakazi wa manispaa, huku lengo likiwa kuwachanja watu milioni 300 ifikapo mwezi agosti mwaka huu.

Kama Shirika la Afya duniani (WHO) pia shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limesaidia katika upande wa mawasiliano na juhudi za uelimishaji ili kuhakikisha usambazaji wa taarifa sahihi kwa wadau na jamii.  Shirika hilo pia limesaidia kuwapa mafunzo wahudumu wa afya ya kuzuia na kudhibiti maambukizi na kutoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto na watu wanaowahudumia.  Mbali ya kusaidia moja kwa moja mchakato wa utoaji chanjo hiyo, mashirika ya Umoja wa Mataifa yameendelea na programu zake za kusaidia jamii zilizo hatarini zaidi ambazo zimeathirika na COVID-19 na athari zinazowakabili za kiuchumi na kijamii.  Kwa mfano shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP limekuwa likiyasaidia mashirika yasiyo ya kiserikali au NGOs kubaini na kusajili kaya zisizojiweza 19,000 na kugawa vifurushi vya chakula, huku shirika la idadi ya watu duniani UNFPA limeendesha programu za uelimishaji hasa katika masuala ya afya ya uzazi na kuzuia ukatili wa kijinsia kwa niaba ya watu milioni 30 walio hatarini.

Ingawa mchakato wa chanjo unaendelea kuhakikisha watu wanakuwa makini na kujikinga dhidi ya COVID-19 ni suala linalosalia kuwa muhimu sana kuliko wakati mwingine wowote.   Kiongozi wa WHO amewataka wahudumu wa afya kuwa makini zaidi katika kufuatilia wagonjwa, kuchunguza, kuwatenga, kuwahudumia na kuwaweka karantini washukiwa ili kuvunja mzunguko wa maambukizi. Daktari huyo pia amehimiza kuhusu masuala matatu muhimu ya kuzingatia ambayo ni kuvaa barakoa, kuawa mikonno  na hakikisha umbali kati ya mtu na mtu. Hatua hizi lazima ziendelee ili kukomesha kusambaa kwa COVID-19. Na  kama watu binafsi na jamii ni lazima washirikiane na serikali kuokoa maisha na uchumi kwa kulingana na hali halisi ya nchi na kwa ulimwengu mzima.

20 January 2021, 16:26