Kukosekana kwa mpango wa IMF nchini Zimbabwe siyo sababu ya kuwaacha watu wateseke zaidi na janga hili.Taifa linahitaji kusaidiwa. Kukosekana kwa mpango wa IMF nchini Zimbabwe siyo sababu ya kuwaacha watu wateseke zaidi na janga hili.Taifa linahitaji kusaidiwa. 

Zimbabwe#coronavirus:Chama cha Kikristo kutoa ombi kwa ajili ya nchi maskini zipokee msaada kujibu janga la sasa!

Chama cha kikristo cha msaada kinaomba kwa haraka ili Zimbabwe ipokee msaada katika kipindi hiki cha dharura ya covid-19.Chama hiki kinaamini kwamba kutengwa kwa nchi hiyo kwenye kifurushi siyo haki,kwa sababu ya hali ngumu ya kiafya iliyosababishwa na Covid-19 na athari zake za kiuchumi kwa watu masikini zaidi na katika mazingira magumu zaidi.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Baada ya kutangazwa wiki iliyopita kwa upande wa mataifa makuu tajiri duniani (G20) kusimamisha kwa muda ulipwaji wa madeni kwa nchi zinazoendelea, kuanzia Mei Mosi hadi tarehe 31 Desemba 2020, Chama cha Kikristo cha kutoa msaada cha Uingereza kinatoa ombi la haraka kwamba Zimbabwe, hata kama haipo kwenye  makubaliano, ipokee misaada inayohitajika  ili kujibu janga la Covid-19.

Kusimamishwa kwa deni hilo, ambalo halitafutwa, lakini lazima lilipwe kati ya mwaka 2022 na 2024, pamoja na riba iliyopatikana kwa muda, inatazama nchi 77 ambazo ni sehemu ya mpango wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa (IDA), wakala ya Benki ya Dunia ambayo inasaidia nchi masikini zaidi ulimwenguni, au zile zenye kipato cha chini. Zimbabwe ni sehemu ya nchi inayoshiriki kwa kijujuu tu katika IDA na  kwa sababu za kiufundi, ilitengwa kwenye mkataba huo. Ikiwa mpango wa sasa wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) umeundwa tena na msaada wa wadau, basi Zimbabwe inaweza kusimamishwa  malipo ya deni kwa upande wa Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika na Benki ya Ulaya kwa uwekezaji, kati ya wadai wengine wa kimataifa.

Chama cha kikristo cha msaada kinaamini kwamba kutengwa kwa nchi hiyo kwenye kifurushi siyo haki, kwa sababu ya hali ngumu ya kiafya iliyosababishwa na Covid-19 na athari zake za kiuchumi kwa watu masikini zaidi na walio katika mazingira magumu zaidi. Kwa maana hiyo wanaomba kwamba Uingereza na serikali nyingine zisaidi sasa kufadhili asasi za kiraia kwa kushirikiana na sekta binafsi, katika kusaidia moja kwa moja masikini, huku wakishughulikia miundombinu, huduma za afya na ulinzi wa vikundi vilivyo hatarini zaidi. Kwa sababu mara tu kesi za Covid-19 zitakapofikia kizingiti fulani, mfumo dhaifu wa afya wa nchi hautaweza kufana hiyo.

Nicholas Shamano, Mhusika wa Cahama cha Kikristo cha msaada nchini Zimbabwe, amesisitiza pia kuwa “kukosekana kwa mpango wa IMF nchini Zimbabwe siyo sababu ya kuwaacha watu wateseke zaidi na janga hili”.  Umuhimu wa kibinadamu kwa sasa ni ule wa kuhakikisha kuwa “jamii ya kimataifa inawasaidia Wazimbabwe kupambana na  athari mbaya za virusi vya corona  na mgogoro wa uchumi duniani”.

22 April 2020, 16:11