Tafuta

Serikali ya Tanzania imesema hadi kufikia tarehe 29 Aprili 2020 wagonjwa 167 wamepona ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona. Wagonjwa wapya ni 196. Serikali ya Tanzania imesema hadi kufikia tarehe 29 Aprili 2020 wagonjwa 167 wamepona ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona. Wagonjwa wapya ni 196. 

Waziri Mkuu Majaliwa: Mwenendo wa Ugonjwa wa Corona Tanzania

Wagonjwa 167 wamepona ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa Virusi vya Corona na ameendelea kuwasisitiza Watanzania wachukue tahadhari ya kutosha na wafuate ushauri wa Wataalamu wa Afya na maelekezo ya Serikali. Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema kuanzia tarehe 23 hadi 28 Aprili, 2020 wamepatikana watu wengine wapya wenye maambukizi ya Corona 196 .

Na Ofisi ya Waziri Mkuu, - Dodoma.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema wagonjwa 167 wamepona ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa Virusi vya corona,COVID-19 na ameendelea kuwasisitiza Watanzania wachukue tahadhari ya kutosha na wafuate ushauri wa Wataalamu wa Afya na maelekezo ya Serikali. Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema kuanzia tarehe 23 hadi 28 Aprili, 2020 wamepatikana watu wengine wapya wenye maambukizi ya Corona 196 (Bara 174 na Zanzibar 22 ambao walitangazwa na Waziri wa Afya wa SMZ) na kufanya jumla ya wenye maambukizi nchini kuwa 480. Waziri Mkuu ametoa taarifa hiyo ya mwenendo wa ugonjwa wa COVID-19 nchini  Jumatano, Aprili 29, 2020 kwenye viwanja vya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma wakati akikabidhi magari ya kubebea wagonjwa kwa wabunge. Pia amesema mbali na magari hayo kutolewa kwa ajili ya kuboresha huduma za mama na mtoto yatatumika kuwahudumia wagonjwa wa COVID-19.

“Tarehe 24 Aprili Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto aliwatangaza jumla ya waliopona kuwa ni 37 na hivyo kufanya jumla ya waliopona kuwa 48. Leo tunafurahi kusema kuwa idadi ya waliopona imeongezeka kutoka 48 na kufikia 167 (Zanzibar 36 waliotanganzwa jana na Waziri wa Afya - SMZ na Bara 83).” “Tunasikitika kueleza kuwa tuna ongezeko la vifo sita na kufanya jumla ya vifo sasa kuwa 16. Hata hivyo kati ya wenye maambukizi 297 waliobaki, watu 283 wanaendelea vizuri sana na watu 14 wako chini ya uangalizi maalum na tunaendelea kuwaondoa walio karibu na wagonjwa (contacts) walio karantini baada ya kumaliza siku 14.” Waziri Mkuu ameongeza kuwa hadi tarehe 28 Aprili, 2020 watu 644 wameruhusiwa, ambao wanatoka katika mikoa ya Zanzibar, Dar-es-Salaam, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Mwanza, Kagera, Dodoma, Kigoma na Songwe.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wananchi wachukue tahadhari kuhusu taarifa za upotoshaji kwani kwa sasa kumeibuka tabia ya watu kutoa takwimu zisizo sahihi kuhusu vifo vitokanavyo na ugonjwa wa COVID-19 ambazo zinasababisha mtafaruku usio wa lazima katika jamii. “…Sio kila kifo ni cha Corona, tunasahau kuwa magonjwa mengine yanaua pia sio kila anayeugua na anayekufa ni corona tuna malaria, BP, kisukari, ukimwi ni magonjwa yanayoua. Tuache tabia ya kupotosha umma. Tuwaache wataalam wetu wafanye kazi zao.” “Kwa wale ambao hawana maambukizi waendelee kufanya kazi zao, mkulima aende akalime tupate chakula cha kutosha, waliko maofini wawajibike kufanya kazi, waliopo viwandani wafanye kazi na kila mmoja na sekta yake kama unafanyabiashara sokoni toa huduma ili wananchi wasikose kupata huduma wanazozihitaji.” Hata hivyo, Waziri Mkuu ameendelea kuwasisiza Watanzania wazingatie maelekezo yanayotolewa na Serikali katika kujikinga na COVID-19 ikiwa ni pamoja na kujiepusha na misongamano. “Tukizingatia makatazo na maeneo yenye tahadhari tutaishinda vita hii dhidi ya ugonjwa huu.”

 

29 April 2020, 14:11