Tafuta

Wazalendo nchini Mali wakiwa wanapiga kura katikati  ya usiku wakiwa wamevaa barakoa. Wazalendo nchini Mali wakiwa wanapiga kura katikati ya usiku wakiwa wamevaa barakoa. 

Mali:#coronavirus:Hatari za kiafya kutokana na covid-19 na ukosefu wa usalama kwa watu wa Mali!

Hatari ya kiafya ya Covid-19 na kutokuwa na usalama kumesababisha watu wa Mali waachane na duru ya kwanza ya uchaguzi kwa upya wa bunge.Kiongozi wa upinzaji Soumaïla Cissé Ijumaa iliyopita alitekwa nyara wakati wa kampeni za uchaguzi nchini humo.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Hofu ya virusi vya corona (CIVID -19)na hatari za kijihad kuhusiana na usalama zimefanya kushuka sana kwa wapiga kura katika duru ya kwanza ya uchaguzi kwa upya wa bunge uliofanyika Dominika tarehe 29 Machi 2020 nchini Mali. Hakuna data rasmi iliyopatikana juu ya kushiriki katika kura, lakini kulingana na Waangalizi wa kikundi cha vyama vya asasi za umma, asilimia 7.5 tu ya wale waliopewa haki walikuwa wamekwenda kupiga kura katikati ya siku. Matokeo ya kwanza yanatarajiwa katika siku kadhaa na mzunguko wa pili ambao umepangwa kufanyika Jumapili 19 Aprili 2020.

Uchaguzi wa uboreshaji wa Bunge umeahirishwa mara kadhaa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita na umefanyika katika mazingira ya kutokuwa na uhakika kwa sababu ya kampeni zote mbili za uchaguzi zilizopunguzwa na hatua za kiafya za corona na utekaji nyara, ambao ulifanyika Ijumaa, kwa kiongozi  Soumalia Cissè, mgombea wa urais tayari kwa mara tatu, na ambaye labda yuko mikononi mwa vikundi vya kijihad vinavyohusika na al Qaeda ambavyo vimekimbilia nchini tangu mwaka wa 2012. Katika maeneo yaliyoathiriwa na vurugu kijihad, vituo vya kupigia kura ni hatua za msingi za makubaliano ya amani

Bunge la sasa liliundwa baada ya uchaguzi wa 2013 na muda wake ulimemalizika tangu 2018, usasishaji wake unaochukuliwa kama hatua  msingi ya kupitisha makubaliano ya amani yaliyosainiwa huko Algiers kunako 2015 kati ya mamlaka na vikundi vya uhuru wa kutumia silaha, vya Tuareg, lakini siyo wanamgambo wa kijihadist.

Mkataba huo unatazama madaraka makubwa zaidi ya madaraka kupitia marekebisho ya katiba. Wapinzani wengine wanaamini kwamba marekebisho hayawezi kupitishwa na Bunge la sasa kwa sababu inachukuliwa na wengi kuwa halali lakini sio halali tena kwa maana hiyo wamebaki kutengwa.

31 March 2020, 09:24