Katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wazazi kimataifa tarehe 1 Juni  Papa anahimiza wazazi wawasaidie watoto kujua upendo wa  Yesu Katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wazazi kimataifa tarehe 1 Juni Papa anahimiza wazazi wawasaidie watoto kujua upendo wa Yesu 

Siku ya Kimataifa ya wazazi:saidieni watoto wagundue upendo wa Yesu!

Tarehe 1 Juni ni maadhimisho ya wiki ya Kimataifa ya wazazi iliyowekwa na Umoja wa Mataifa kunako 2012. Katika tweet ya Papa anawaalika wazazi wawasaidie watoto wao kugundua upendo wa Yesu.Na kwa mujibu Per Pietro Boffi wa kituo cha mafunzo ya kimataifa kuhusu familia anamethibitisha kuwa masuala ya nafasi ya mama na baba katika jamii ni msingi katika nyakati hizi.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Wapendwa wazazi, saidie watoto wenu ili wagundue upendo wa Yesu! Hiyo itawafanya wawe na nguvu na ujasiri, ndiyo ujumbe wa maneno yaliyomo katika tweet ya Baba Mtakatifu Francisko tarehe 1 Juni 2019 wakati wa kilele cha Siku ya Kimataifa ya wazazi, iliyotangazwa na Umoja wa Mataifa kunako mwaka 2012 kwa azimio la A/RES/66/292 ili kuheshimu wazazi wote duniani. Siku ya Kimataifa ya wazazi ni fursa kwa ajili ya kuwapongeza wazazi wote duniani katika  jitihada zao za bure na zisizo na kikomo mbele ya watoto na  wale wote ambao daima wanaendelea kutoa sadaka yao kukuza uhusiano wa watoto hao. Tendo la kuwa wazazi wema kama wa mama na  baba ambao wanaheshimiana pamoja ni msingi kwa ajili ya mafunzo ya watoto kwa njia ya mioyo ya sadaka ambayo ni muhimu zaidi kwa ajili ya matumaini makubwa katika  jumuiya ya kimataifa inayojitahidi kutimiza”. Haya ni maneno yaliyokuwa yametamkwa na Askofu Mkuu Bernadito Auza, Mwakilishi wa kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa wakati wa hotuba yake katika fursa ya siku hiyo mwaka 2018.

Maana  ya siku  hii; umuhimu wa kusaidia familia

Siku ya wazazi ilizaliwa kama fursa ya kupongeza wazazi wote duniani kote na kuwashukuru kwa ajili ya jitihada zao mbele ya watoto na sadaka zao. Kuanzia miaka ya 80 familia ilianza kupata umuhimu mkubwa katika jumuiya ya kimataifa, hata katika uwajibikaji msingi wa elimu na ulinzi wa watoto na kuwafanya waendelee kukua binafsi kwa namna kamilifu na muungano. Hata hivyo umuhimu wa kusaidia familia unaweza kuleta mwafaka kwani, sera za kisiasa zinazolenga katika familia, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa zinaweza kutoa mchango mkubwa wa kuondoa umasikini na njaa, wakati huo huo  wakihamasisha ustawi wa kila wakati, katika maendeleo ya binadamu na zaidi kuhakikisha mafunzo msingi ya kuweza kufikia hali ya usawa kwa ujumla

Umuhimu msingi wa wazazi na ushirikishwaji katika uwajibikaji wa wazazi

Umuhimu wa wazazi leo hii kwa hakika  ni muhimu kulingana miaka iliyopita, kwa sababu ya ugumu ambao upo katika masuala ya kijamii, kiutamaduni na desturi ya wazazi, pia ni jukumu hasa la mgogoro kutokana na shida ya kuwa na mamlaka bila kuwa na madaraka. Kwa upande wa Italua taarifa inaasema kuwa wamefikia kuwa na  shida kubwa ya kuanzisha kwa baba mmoja na  mpya au siku mbili (zaidi ya tatu, lakini mwaka ujao) kuna ulazima na ambao bado ni msingi ili baba waweze kuwapo na kuwa watatu hasa katika wanandoa wakati mtoto anapokuwa anazaliwa. Wajibu wa wazazi, hasa katika siku chache za kwanza za uhai wa mtoto zinapaswa zichukue nafasi kuu  kwa namna inayoshirikishwa na baba mbele ya wamama.

Lengo la agenda 2030 ya maendeleo endelevu

Malengo makuu ya Agenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu, iliyopitishwa na viongozi wa dunia mwaka 2015, yanalenga kuimarisha umasikini, kukuza na kugawana ustawi wa uchumi, maendeleo ya kijamii na ustawi wa watu, wakati huo huo wa kulinda mazingira. Familia hubakia kuwa kitovu cha maisha ya kijamii na kuhakikisha ustawi wa kila mwanachama, kuelimisha na kuingilia wavulana na wasichana na kutunza vijana na wazee. Wazazi wa kila kabila, dini, utamaduni na taifa duniani kote ni wa kwanza kuwatunza na kuelimisha watoto, ba  kuwaandaa katika maisha ya furaha, yenye kuzaa na mazuri. Wazazi wanakuwa ni nanga ya familia na msingi wa jumuiya zetu na jamii zetu.

Haki za wazazi na watoto.

Kanuni zilizotajwa katika mfumo wa haki za binadamu zinatumika kwa watoto na watu wazima. Watoto wanaelezewa wazi katika zana nyingi za kulinda haki za binadamu; viwango vinabadilishwa hasa, au kubadilishwa, ambapo mahitaji na wasiwasi zinazohusiana na haki ni tofauti kwa watoto. Mkataba wa Haki za Mtoto unachanganya na haki za binadamu za watoto na katika vyombo vingine vya ulinzi wa kimataifa. Mkataba huu unaonyesha haki zaidi kabisa na hutoa mfululizo wa kanuni zinazoongoza zinazotoa mambo muhimu kwa maono ya watoto. Watoto wote wana haki sawa. Haki zote zinaunganishwa na zina umuhimu sawa. Mkataba unasisitiza kanuni hizi na inahusu wajibu wa watoto kuheshimu haki za wengine, hasa wazazi wao. Vile vile, ufahamu wa watoto kuhusu masuala yaliyotolewa katika Mkataba utatofautiana kulingana na umri. Kuwasaidia watoto kuelewa haki zao haimaanishi kuwa wazazi wanapaswa kuwafukuza kufanya uchaguzi na matokeo ambayo hawataweza kusimamia wakati wao.

Mababa: Katika utamaduni wa jamii nyingi, baba anaendelea kutunza familia na ni mwalimu wa maadili na wa madaraka. Siku hizi, katika Mataifa mengi kuna msisitizo mkubwa juu ya jukumu la baba kama mzazi-mwenza, akihusisha kikamilifu katika mambo ya kihisia ya kila siku ya kumlea mtoto. Uchunguzi wa hivi karibuni umethibitisha matokeo mazuri ya yanayojikita kuhusu uhai  baba katika maendeleo ya watoto. Mama: Mama ana jukumu msingi ndani ya familia, ambayo ni nguvu kubwa ya ushirikiano wa kijamii na ushirikishwaji. Uhusiano wa mama na mtoto ni muhimu kwa maendeleo ya afya ya mtoto. Vurugu dhidi ya wanawake, wengi wao ni mama, lakini ambayo bado ni mojawapo ya ukiukwaji wa haki za binadamu mkubwa zaidi wakati wetu. Faida za kuelimisha wanawake na wasichana sio faida tu kwa ajili ya  familia binafsi, lakini pia jamii nzima, kwa kuipa uwezo wa wanawake kuchangia katika jitihada za kubwa za maendeleo. Takwimu zinaonyesha pia kwamba mama wenye elimu wanapenda watoto wao wabaki shuleni, na ambayo inamaanisha kuwa faida za elimu inazidi vizazi.

03 June 2019, 10:29