Tarehe 9 Juni wimbi la watu wamefanya maandamano makubwa huko Haiti wakitaka rais Jovenel Moise ajiuzuru Tarehe 9 Juni wimbi la watu wamefanya maandamano makubwa huko Haiti wakitaka rais Jovenel Moise ajiuzuru 

HAITI:Ujumbe wa maaskofu kuhusu kesi ya Petrocaribe ni kupambana na rushwa na kushtaki wafisadi!

Kufuatia na maelfu ya watu wa Haiti kushuka barabara za mji mkuu tarehe 9 Juni 2019,wakitaka Rais Jovenel Moïse ajiuzuru,Maaskofu wametoa ujumbe kuhusiana na kesi ya Petrocaribe wakiomba raia na viongozi wote waweze kupambana na rushwa na zaidi kushtaki wahujumu wa rushwa kisiwani humo.Watu wengi wanateseka na matokeo na madhara ya matendo ya ufisadi.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Mamia elfu ya watu wa Haiti wameshuka  kuandamana katika bararaba ya mji Mkuu  tarehe 9 Juni 2019 wakiomba Rais wa Haiti Jovenel Moïse ajiuzuru. Kwa mujibu ripoti za  Mahakama Kuu kitengo cha Wakaguzi na Utawala wa Madai kuhusu mahesabu yeye ni mhusika wa matumizi mabaya ya fedha na kupotea kwa fedha za PetroCaribe siku chache zilizopita. Kuhusiana na mahesabu, Mahakama Kuu imetoa ripoti yenye zaidi ya kurasa 600 juu ya uendeshaji wa Petrocaribe, ambao ni mpango wa maendeleo unaofadhiliwa na Venezuela, kwa kutoa ufafanuzi ulio wazi kuhusu idadi kubwa ya kesi za undeshaji kiholela wa fedha na rushwa zenye kufikia maelfu na maelfu ya dola za kimarekani. Kufuatia na suala hili, Baraza la Maaskofu wa Haiti (CEH) katika ujumbe wao uliotiwa sahini na Askofu  Launay Saturné, wa Jimbo Katoliki la Jacmel na Rais wa Baraza la Maaskofu wa Haiti (CEH) pamoja na maaskofu wote wa (CEH) wamejibu kwa sauti kali mbele ya kesi hii mpya ya matumizi mabaya ya fedha. Maaskofu wanasema: “Tumesoma kwa uangalifu na kuwa na  mtazamo wa taarifa mbili za ukaguzi zilizo tolewa na Mahakama Kuu ya Wakaguzi na Utawala wa Madai (CSC/CA) juu ya usimamizi wa mipango iliyo fadhiliwa na fedha za PetroCaribe”.

Ukubwa na ubaya wa rushwa

Maaskofu wa Haiti, wanasema, mpango  huu ni mwanga ulio wazi na mkubwa juu ya jambo kubwa na la kushangaza kuhusiana na  ubaya wa rushwa katika njia zake mbalimbali hasa za kisiasa na za uendeshaji. Rushwa iliyojumuishwa inageuka kuwa ubaya wa mwisho kiukweli uliosababisha na wizi uliopangwa. “Imekuwa ni janga la kweli la kijamii ambalo linasumbua taasisi zetu na kwa hiyo linadhoofisha sana wote kutokana na mtazamo wa kimaadili na kiuchumi na maendeleo ya nchi yetu.  Wanasema maaskofu: watu wa Haiti wanatarajia taarifa hizi mbili za udhibiti zilizotolewa na CSC / CA kufuatiliwa. Katika ghadhabu na kashfa kubwa ya rushwa inayofikia au kubomoa kilele cha serikali, wanaomba kesi ya PetroCaribe itiliwe maanani. Vile vile Maaskofu wa Haiti wanabainisha kuwa nchi yao  imekuwa na mfumo maskini zaidi kutokana na tamaa za viongozi walaruaji na ambao hawana uwezo wa kutazama hali halisi ya watu na matatizo yao. Viongozi hao hawasaidii maendeleo ya nchi. Watu  wako wanateseka na matokeo hayo …na madhara ya matendo hayo… kwa sababu ya ukosefu wa msimamo wa kisiasa  na wakati huo huo kugeuka nyakati za ulevi wa mauaji bila kikomo. Kwa hakika wanateseka katika sekta zote za maisha kitaifa na zaidi ghasia zinamkumba kila mmoja, wanaandika.

Ni wakati wa kuwajibika

Hata hivyo katika ujumbe wao, Maaskofu wa Haiti wanakumbusha kuwa haisadii kuhesabu yote hayo, badala yake kinacho takiwa ni uwajibikaji. Muda umetimia sasa wa kufanya mabadiliko, hasa mbadiliko ya kina… wanaomba wazalendo wajaribu kubainisha wale ambao kweli wanajaribu kutafuta wema wao. Hiyo ni kutokana na kwamba mambo yanabadilika; ni ya lazima na kwa ngazi zote za utawala, katika maofisi, wanawake na wanaume wapya katika akili yao na katika dhamiri yao ya kitaaluma na uwezo wao.  Hilo ndiyo lengo ambalo wameamua kuingilia katika ili viongozi wa kisiasa wawe mstari wa mbele katika uwajibikaji wao. Wanawashauri waweze kutafuta namna ya kurudisha haki kijamii na kujiwakilisha katika haki ya nchi na mbayo ni gharama kubwa kurudisha maadili ya utawala katika Serikali na viongozi wake!

11 June 2019, 14:33