Tafuta

LIBERIA-AFRICA-EDUCATION LIBERIA-AFRICA-EDUCATION 

Utofauti wa elimu,afya na kipato vinaongeza pengo la usawa!

Ripoti mpya kuhusu maendeleo ya binadamu iliyotolewa 14 Septemba, inasema Norway, Uswisi, Australia, Ireland na Ujerumani ziko nafasi ya juu, na hali nafasi za chini kabisa zikishikiliwa na Syria, Niger, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudan Kusini, Chad na Burundi. Mizozo na mapigano imetajwa kuwa ndiyo sababu kuu ya nchi hizo kushika nafasi za chini zaidi katika elimu na maendeleo

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Pengo kubwa la usawa kati ya ustawi wa binadamu unarudisha nyuma maendeleo ya ustawi wa binadamu, imesema ripoti mpya kuhusu kipimo cha maendeleo ya binadamu, HDI, iliyotolewa tarehe 14 Septemba 2018 mjini New York, Marekani na shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP. Ripoti hiyo inapima mafanikio katika kuboresha afya, elimu na kipato ikihusisha nchi 189 zikipangwa kuanzia ya juu kabisa yenye nafasi nzuri hadi ya mwisho.

Mataifa ambayo bado yamedorora: Norway, Uswisi, Australia, Ireland na Ujerumani ziko nafasi ya juu, na  hali nafasi za chini kabisa zinashikiliwa na Syria, Niger, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudan Kusini, Chad na Burundi. Mizozo na mapigano imetajwa kuwa ndiyo sababu kuu ya nchi hizo kushika nafasi za chini zaidi.

Akizungumzia ripoti hiyo, Mtawala Mkuu wa UNDP, Achim Steiner amesema kuwa, “kwa wastani mtoto anayezaliwa leo katika nchi yenye maendeleo duni ya binadamu anatarajiwa  kuishi takriban miaka 60,wakati mtoto wa nchi ambayo watu wake wameendelea anaweza kuishi hata  miaka 80.”

 Kuna mafanikio yoyote?: Hata hivyo kuna mafanikio hususan katika nchi za Afrika zilizo kusini mwa jangwa la Sahara, pamoja na   Asia ya Kusini, huduma za zinaonekana kuwa zimeimarika  kwa kuzingatia kuwa kiwango cha kuishi pindi mtu anapozaliwa kimeongezeka kwa asilimia 11 wakati katika maeneo mengine ni asilimia 7. Halikadhalika kati ya mataifa 189 yaliyohusishwa   59 kati ya hayo  kwa sasa yako katika kundi la mataifa yaliyo na kiwango cha  juu na ni mataifa 38 tu ambayo yameshuka hadi kiwango cha chini kwenye kipimo hicho cha maendeleo ya binadamu kwa mwaka huu wa 2018.

Hali ya sasa: Kwa mujibu wa ripoti hiyo idadi hiyo ni mafanikio makubwa kwa kuwa  takriban miaka minane iliyopita ni mataifa 46 tu ndiyo yalikuwa juu huku mataifa ya kiwango cha chini yalikuwa  49. Miongoni mwa mataifa ya kiafrika ambayo yanapanda kimaendeleo ni Botswana ambayo ilipanda juu nafasi nane, ikilingana na Uturuki pamoja na Jamhuri ya Dominica. Kuhusu tofauti za kijinsia ,ripoti inasema kumeonekana maendeleo  ya kujaribu kuziba pengo kati ya jinsia zote wakati wa umri mdogo lakini pengo linaongezeka wanapokuwa watu wazima.

Imetoa mfano kuwa katika sekta ya nguvu kazi duniani bado idadi ya wanawake ni asilimia 49 ikilinganishwa na asilimia 75 ya wanaume ukosefu wa elimu ukitajwa moja ya sababu zinazokwamisha wanawake kusonga mbele. Kuhusu mchango wa wanawake kushiriki katika siasa za ubunge, idadi ya wanawake bado ni ndogi ingawa ripoti inasema inatofautiana kikanda ambapo katika bara Asia wanawake huchukua asilimia 17.5 na Uarabuni asilimia 18.

 

14 September 2018, 14:04