Tafuta

2023.10.10 Dk.Ruffini,Sr Echeverri na Kardinali Tobin wamezungumza na waandishi wa habari kuhusu Sinodi. 2023.10.10 Dk.Ruffini,Sr Echeverri na Kardinali Tobin wamezungumza na waandishi wa habari kuhusu Sinodi. 

Sinodi,Kanisa zuri ni Kanisa lenye milango iliyofunguliwa

Katika mkutano na waandishi wa habari Oktoba 10,Rais wa Tume ya Habari,Dk.Ruffini,alitoa sasisho juu ya kazi ya vikundi vidogo kwenye sehemu ya pili ya Instrumentum laboris.Kadinali Tobin wa Marekani alizungumzia juu ya utajiri wa kulinganishwa kwa uzoefu na tamaduni,huku Sr. Echeverri wa Colombia akazungumzia kuhusu wito wa kusikiliza kilio cha maskini.

Na Alessandro Di Bussolo & Angella Rwezaula,- Vatican.

Uzuri wa kweli wa Kanisa Katoliki unaonekana wazi wakati milango yake iko wazi na kuwakaribisha watu. Tunatumaini kwamba Sinodi itatusaidia kuzifungua zaidi. Hivyo ndivyo Kadinali Joseph William Tobin, Askofu Mkuu wa Newark, nchini Marekani alivyoeleza mada ya sehemu ya pili ya Instrumentum laboris au kitendea kazi. Sehemu hiyo inabainisha wazi mada ya: "Ushirika unaong’aa: Tunawezaje kuwa ishara kamili zaidi na chombo cha umoja na Mungu na umoja wa wanadamu wote?" ambayo ilijadiliwa katika vikundi vidogo  vidogo Jumatatu tarehe 9 Oktoba mchana na Jumanne asubuhi tarehe 10 Oktoba 2023 katika Sinodi inayoendelea. Kardinali Tobin alizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu kazi ya mkutano huo ulioongozwa na Rais wa Tume ya Habari, Dk. Paolo Ruffini, na Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano.

Dk. Paulo Ruffini,Rais wa Tume ya Habari ya Sinodi na Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano
Dk. Paulo Ruffini,Rais wa Tume ya Habari ya Sinodi na Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano

Makabiliano katika vikundi vidogo vidogo katika sehemu ya pili

Katika vikundi vidogo vidogo, washiriki wa Mkutano Mkuu walijadili elimu, mazingira, tamaduni nyingi na kutembea na watu waliotengwa na wahamiaji. Siku ya Jumatatu 9 Oktoba 2023, walichagua wajumbe wa Tume ya Ripoti ya Muswada na wale wa Tume. Vikundi vidogo vidogo vilivyopangwa kwa msingi wa mada zinazoshughulikiwa, vilijadili vifungu vidogo vya hati hiyo B1 vilivyojikita juu ya  ushirika na vitawasilisha tafakari yao katika mkutano mkuu wa tano mchana na katika kusanyiko la sita na la saba Jumatano asubuhi tarehe  11 Oktoba 2023.

Dk. Ruffini: ushirikiano mkubwa kati ya washiriki wote

Akijibu maswali ya waandishi wa habari, Dk. Ruffini alisisitiza kuwa katika Sinodi  ya tatu, wajumbe wana fursa nyingi zaidi za kuzungumza, hasa katika vikundi vidogo. "Kuna ushirikiano mkubwa kati ya washiriki wote, kulingana na uzoefu wangu binafsi, mbayo ilianza na mafungo ya kabla ya sinodi." Kardinali Tobin kwa upande wake akijibu swali kuhusu Sinodi hiyo kuelekezwa kutoka juu kwenda chini alisema kwamba, “anajiamini kwa sababu mambo hayatujii kutoka juu bali ni mchakato unaoanzia chini kuanzia  na uhusika wa Watu wa Mungu, na kufika kileleni. Sijisikii kulazimishwa au kufungwa pingu,”alisisitiza Kardinali huyo.

Sr. Echeverri Rais wa Shirikisho la Mashirika ya Kitawa Amerika Kusini na mjumbe wa Sinodi
Sr. Echeverri Rais wa Shirikisho la Mashirika ya Kitawa Amerika Kusini na mjumbe wa Sinodi

Sr. Echeverri: Tunasikiliza kilio cha maskini, wahamiaji na waliotengwa

Mbali na Kardinali Tobin Mtawa wa Shirika la Mkombozi na mjumbe wa Baraza la Kawaida la Sekretarieti ya Sinodi, kulikuwa na Sista Gloria Liliana Franco Echeverri, kutoka Colombia wa Shirika la Bikira Maria, na rais wa Shirikisho la Watawa wa Amerika  Kusini (CLAR) na ambaye ni  shuhuda  wa Mchakato wa Sinodi. Kama kawaida, pia Sheila Leocádia Pires, katibu wa Tume ya Habari ya Sinodi, pia alizungumza. Kwa njia hiyo akizungumza Sr. Echeverri alisisitiza kwamba miongoni mwa washiriki wa Mkutano Mkuu wa XVI wa Kawaida wa Sinodi ya Maaskofu, kuna nia ya kuishi kama Yesu “Anayefanya ubinadamu, Anayeheshimu, Anayejumuisha, Yesu anayefungua mlango kwa ajili ya mwingine.”

Kardinali Tobin Askofu Mkuu wa Newark,nchini Marekani
Kardinali Tobin Askofu Mkuu wa Newark,nchini Marekani

Sr. huyo aliendelea kusema kuwa ni mchakato “unaoona njia tofauti, kuanzia na kuongoka katika Roho. Katika vikundi vyetu vidogo tunatambua kwa usahihi hadhi hii ya pamoja, hadhi inayotokana na heshima, ushirika na kutambuliwa kwa pande zote. Katika mjadala juu ya sehemu ya sasa, “inayovuma mioyoni mwetu ni wito wa kusikiliza kilio cha maskini. Katika meza yetu, sura ya maskini, uhamiaji, biashara haramu ya watu, kutengwa na jamii katika pembezoni kulisikika kwa sauti kubwa,” alithibitisha.

Kardinali Tobin: kuvutia kwa mazungumzo katika tamaduni nyingi

Kadhalika Kardinali Tobin, ambaye yuko katika kikundi kidogo  pamoja na  Sr. Echeverri, alielezea tena kwamba msichana kutoka Urussi, mama kutoka Ukraine na mchungaji wa Kipentekoste kutoka Ghana, mtaalimungu kutoka Malaysia na mratibu kutoka Singapore pia walikuwa katika kundi lao. “Ni hali bora kwangu, kuwa katika kundi la watu mbalimbali na kuweza kuwasikiliza wengine. " Hilo, alisema lilimvutia, kwa kuwa alikulia huko Detroit katika mazingira ya kiutamaduni, na ambaye kama kasisi kwa miaka 45 ameishi katika tamaduni ambazo hazikuwa zake, na hata ile aliyolelewa. Kwa njia hiyo alibainisha kwamba hiyo ni kama "Sinodi tofauti zaidi ambayo nimewahi kushiriki."

Sheila Leocádia Pires, katibu wa Tume ya Habari ya Sinodi
Sheila Leocádia Pires, katibu wa Tume ya Habari ya Sinodi

"Chaguo la Kanisa ni udugu: kuna nafasi kwa kila mtu"

Kardinali Tobin pia alishirikisha tukio halisi la kichungaji, mapokezi katika Kanisa Kuu la Newark kuhusu "hija ya watu waliohisi kutengwa kwa sababu ya mwelekeo wao wa kijinsia." Hiyo, alisema, ilikuwa tukio la wazi la Kanisa. Na alihitimisha kwamba katika ulimwengu unaodhihirishwa na utaifa wa kutengwa, na chuki dhidi ya wageni, ambapo kuna viongozi ambao wamejitolea kujenga mipaka, chaguo la Kanisa ni udugu, sinodi, ambalo ni chaguo linalotuwezesha kuelewa kuwa sisi sote ni kaka na dada. Kwa hiyo katika Kanisa ambalo tunajiona kama kaka na dada kuna nafasi kwa kila mtu, alisema Kardinali Tobin.

Wakati wa kuwasilisha yatokanayo ya Sinodi kwa waandishi wa habari
Wakati wa kuwasilisha yatokanayo ya Sinodi kwa waandishi wa habari
10 October 2023, 19:00