Tafuta

2023.09.18  Kitabu kilichochapishwa na  LEV cha Riccardo Bonacina Nitakutunza." Kinahusu mafundisho ya Papa Francisko kwa miaka kumi ya upapa wake. 2023.09.18 Kitabu kilichochapishwa na LEV cha Riccardo Bonacina Nitakutunza." Kinahusu mafundisho ya Papa Francisko kwa miaka kumi ya upapa wake. 

Nitakutunza ni kitabu cha maneno Papa kuhusu kujitolea

Kitabu kilichochapishwa na LEV na Solferino na kuhaririwa na Riccardo Bonacina kuhusu wito wa manufaa ya wote,ambayo kupitia hotuba,mahubiri na hati zingine,inafuatilia moja ya nguzo za mafundisho ya Papa Francisko:Kitabu kinahifadhi aina ya katekesi juu ya mwelekeo kuelekeza wengine.

Vatican News

Kitabu kilichochapishwa na Nyumba ya Vatican  LEV na Solferino kinaitwa ‘Nitakutunza. Wito kwa manufaa ya wote’, ambapo kitakuwa katika maduka ya vitabu  kuanzia tarehe 19 Septemba 2023. Ni aina ya ‘Katekesi’ kama alivyoeleza mtunzi Riccardo Bonacina. Kwa hakika, kinakusanya matamshi yote ya Papa Francisko katika miaka hii kumi ya Upapa wake  juu ya mada kuu ya kuwakaribisha wahitaji. Ni mada ya sasa sana, ambayo kama inavyoonesha katika kichwa kidogo kinakumbusha mzizi wa  chimbuko la ujenzi wa wema kwa wote, unaoakisi mtazamo wa kiinjili wa kila mwamini.

Nadharia yake ni kwamba Papa ambaye alitoka Argentina kwa wakati fulani alithibitisha  kuwa amejua uzuri wa  watu wa kujitolea sana  nchini Italia na kwa hiyo mtunzi wa  kitabu  Bonacina  anabainisha kuwa hilo ni chaguo la bure kwa wengine ambalo lina sifa ya utamaduni wa nchi ya Italia  na ambayo inajidhihirisha hasa katika hali za dharura. “Kiukweli tumeiona katika janga la Uviko na vile vile katika matukio mengine kwa mfano ya hivi karibuni  ya  mafuriko ya Emilia Romagna hadi tetemeko la ardhi huko Morocco na kwingineko.”

Bila chaguo hili la bure, manufaa ya wote yatasambaratika, amesisitiza mtunzi wa kitabu Bonacina, huku akifafanua jinsi ambavyo kama kitabu kinavyozungumzia juu ya hotuba za Papa wakati wa Katekesi zake, kwa mikutano, vyama, mashirika, Barua za kitume hata mikutano mingine ya umma.

Kitabu cha Nitakutunza kinaelezea mafundisho ya Papa
18 Septemba 2023, 18:01