Tafuta

Mtakatifu Rita wa Cascia:Kila tarehe 22 Mei, Mama Kanisa anamkumbuka Mtakatifu wa mambo yasiyowezekana. Mtakatifu Rita wa Cascia:Kila tarehe 22 Mei, Mama Kanisa anamkumbuka Mtakatifu wa mambo yasiyowezekana. 

Kard.Semeraro:Mtakatifu Rita alipata shahada ya upendo

Katika mahubiri ya KardinaliSemeraro,Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Kuwatangaza Watakatifu katika Sikukuu ya kiliturujia ya Mtakatifu wa Cascia alisema kwamba Mtakatifu huyo alieneza amani iliyopendwa na kufuatiliwa kama wema mkuu,upendo wa kidugu na wa dhati katika kumtumaini Mungu.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Mwanamke, mtakatifu, aliyejulikana kwa mateso lakini ambaye bado leo hii, baada ya karne nyingi ni kielelezo cha furaha kwa waamini wote. Ndivyo Kardinali Marcello Semeraro, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Kuwatangaza Watakatiu alisema katika kukumbukuka Mtakatifu Rita wa Cascia, anayejulikana duniani kote, anayependwa  na ambaye kumbukumbu yake ya kiliturujia inaadhimishwa kila ifikapo tarehe 22 Mei ya kila mwaka. Kardinali Semeraro aliongoza Misa Takatifu katika Madhabahu ikafuatia sala na baraka ya mawaridi.

Masali ya Mtakatifu Rita wa Cascia
Masali ya Mtakatifu Rita wa Cascia

Katika mahubiri yake, Kardinali  Semeraro alieleza alivyojitayarisha kwa ajili ya maadhimisho hayo kwa kuchukua maandishi kutoka  Jalada la Kumbukumbu  ya  maisha ya Mtakatifu huyo (Positio super virtutibus) yaliyochapishwa mnamo mwaka 1897 kwa ajili ya kumtangaza Rita kuwa mtakatifuna ambao ni muhtasari wa historia yake kwa kuanzia na wito kwa nyuki, tangu mwanzo waliopo katika mila ya Rita. “Nyuki, wakiviviringisha vinywani mwao wanatabiri kwamba maneno yake yangekuwa matamu kama asali. Mara baada ya hapo, wimbo unakumbuka jinsi alivyoingia, kwa namna ya kielelezo, hali mbalimbali za maisha ya Kikristo: uchumba, ujane na maisha ya kuwekwa wakfu. Baadaye kuna kumbukumbu ya muujiza wa donda ambao  hasa Msalaba uliojibu maombi yake kwa kumpa moja ya miiba ya taji lake, alisema Kardinali Semerao na kwamba Shahidi, mmoja alisema kuwa Rita alipata hamu ya kweli ya kuwa sehemu ya maumivu yale ambayo Yesu alitaka kuteseka kwa ajili ya upendo wetu.

Mawaridi katika Madhabahu ya Kanisa la Cascia
Mawaridi katika Madhabahu ya Kanisa la Cascia

Kadinali  Semeraro  vile vile alikumbuka  maneno ya Mtakatifu  Yohane Paulo wa Pili aliyoandika wakati wa kuadhimisha karne ya sita ya kuzaliwa kwa Mtakatifu huyo kwamba “Ishara ya mwiba, zaidi ya mateso ya kimwili ambayo ilimsababishia, ilikuwa katika Mtakatifu Rita kama muhuri wa maumivu yake ya ndani; hata zaidi, hata hivyo, ulikuwa uthibitisho wa kushiriki kwake moja kwa moja katika Mateso ya Kristo”. Na tena aliandik: “Donda  linalong’aa kwenye paji la uso wake ni uthibitisho wa ukomavu wake wa Kikristo. Msalabani pamoja na Yesu, kwa namna fulani alihitimu katika upendo huo, ambao tayari alikuwa ameujua na kuuonesha kwa njia ya kishujaa ndani ya kuta za nyumba yake na kushiriki katika matukio ya jiji lake”.

Mahujaji huko Cascia kwa Mtakatifu Rita
Mahujaji huko Cascia kwa Mtakatifu Rita
Mtakatifu Rita wa Cascia
23 May 2023, 17:02