Tafuta

Tovuti mpya ya Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na vyama vya kitume imezinduliwa ili kuwezesha upatikanaji wa habari kuhusu baraza na hati mbali za kipapa na Baraza. Tovuti mpya ya Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na vyama vya kitume imezinduliwa ili kuwezesha upatikanaji wa habari kuhusu baraza na hati mbali za kipapa na Baraza.  (Vatican Media)

Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa wako tayari na tovuti

Toleo jipya la mtandaoni,katika lugha kadhaa,kwa njia ambayo habari,nyaraka na machapisho yanaweza kupatikana kwa urahisi.Jibu kwa mwaliko uliotolewa na Papa wa kutafuta njia mpya na njia za kusaidia mawasiliano ya kikanisa katika tangazo la ajabu ambalo linaitwa kuletwa katika milenia ya tatu.

Na Angella Rwezaula- Vatican.

Tovuti mpya ya Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na vyama vya Kitume sasa liko mtandaoni (www.vitaconacrata.va). Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Baraza hilo  la Kipapa ni kwamba Tovuti, katika toleo lake jipya kabisa linalenga kuwa chombo cha mawasiliano na habari kwa kila mtu, hasa kwa wanaume na wanawake waliowekwa wakfu.

Ufikiaji wa haraka wa habari

Tovuti hiyo  inakusanya habari, shughuli, nyaraka na machapisho ya Baraza lenyewe. Mbali na nyenzo na marejeo, pia ina baadhi ya machapisho ya Baraza hilo katika lugha mbalimbali, kuanzia barua kwa wanaume na wanawake waliowekwa wakfu zinazotolewa kwenye mwadhimisho ya kila  Mwaka wa Siku ya  Watawa  duniani na nyaraka nyingine za Kipapa. Kwa hiyo, Injini ya utaftaji kwenye ukurasa wa nyumbani hunakuruhusu kupata habari zote kwa haraka.

Ishara ya ukaribu na kushiriki

Tovuti hiyo pia inataka kuwa ishara ya ukaribu na ushirikiano ambapo Baraza la Kipapa hilo linakusudia kukubali mwaliko wa Papa, uliotolewa na Papa Francisko katika Ujumbe wa Siku ya Mawasiliano Duniani 2023: “Nina ndoto ya mawasiliano ya kikanisa ambayo yanajua jinsi ya kujiruhusu kuongozwa na Roho Mtakatifu, mpole na wakati huo huo wa kinabii, ambaye anajua jinsi ya kupata aina mpya na njia za tangazo la ajabu ambalo ameitwa kuleta kwenye milenia ya tatu”, alisisitiza Papa katika ujumbe wake hivi karibuni.

Toleo Jipya la Tovuti ya Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na vyama vya kitume
29 May 2023, 11:04