Tafuta

Rais Alassane Ouattara wa Pwani ya Pembe amekutana na viongozi wakuu wa Vatican tarehe 17 Septemba 2022. Rais Alassane Ouattara wa Pwani ya Pembe amekutana na viongozi wakuu wa Vatican tarehe 17 Septemba 2022. 

Rais wa Pwani ya Pembe Akutana na Kuzungumza na Papa Francisko

Baba Mtakatifu na mgeni wake, wameridhishwa na uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili. Baadaye wamezama katika masuala ya kijamii na kiuchumi, hasa katika mchakato wa umoja na upatanisho wa Kitaifa. Wamepongeza mchango unaotolewa na Kanisa Katoliki nchini Pwani ya Pembe kwa ajili ya ustawi, maendeleo na mafao ya wengi, hususan katika sekta ya elimu na afya.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. – Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi tarehe 17 Septemba 2022 amekutana na kuzungumza na Rais Alassane Ouattara wa Jamhuri ya Watu wa Pwani ya Pembe, “Ivory Coast” na baadaye, Rais amekutana pia na kuzungumza na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa Mambo ya Nchi za Nje, Ushirikiano na Mashirika ya Kimataifa

Vatican na Pwani ya Pembe wameridhishwa na uhusiano wao wa kidiplomasia
Vatican na Pwani ya Pembe wameridhishwa na uhusiano wao wa kidiplomasia

Katika mazungumzo yao, Baba Mtakatifu na mgeni wake, wameridhishwa na uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili. Baadaye wamezama zaidi katika masuala ya kijamii na kiuchumi, hasa katika mchakato wa umoja na upatanisho wa Kitaifa. Wamepongeza mchango unaotolewa na Kanisa Katoliki nchini Pwani ya Pembe kwa ajili ya ustawi, maendeleo na mafao ya wengi, hususan katika sekta ya elimu na afya. Katika mazungumzo yao, viongozi hawa wawili wamebadilishana mawazo kuhusu masuala ya Kimataifa na Kikanda kwa kufanya rejea kuhusu jinsi hali ilivyo Magharibi mwa Afrika, Ukanda wa Sahel; Ulinzi na usalama katika eneo hili.

Papa Pwani ya Pembe

 

17 Septemba 2022, 17:50