Tafuta

Rais Wiliame Katonivere wa Fiji tarehe 1 Agosti 2022 amekutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican. Rais Wiliame Katonivere wa Fiji tarehe 1 Agosti 2022 amekutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican.  (Vatican Media)

Rais wa Jamhuri ya Watu wa Fiji Akutana na Kuzungumza na Papa Francisko Mjini Vatican

Papa Francisko pamoja na Rais wa Jamhuri ya watu wa Fuji katika mazungumzo yao ya faragha, wamegusia masuala ya Kimataifa na Kikanda, lakini kwa namna ya pekee kabisa, umuhimu wa kusimama kidete kulinda, kutunza na kudumisha mazingira nyumba ya wote, kwa sababu madhara yake kwa ustawi, maendeleo na mafao ya wengi ni makubwa sana. Mchango wa Kanisa Fiji!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. – Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 1 Agosti 2022 amekutana na kuzungumza na Rais Ratu Wiliame Maivalili Katonivere wa Jamhuri ya Watu wa Fiji, ambaye baadaye amepata fursa ya kuzungumza na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekua ameambatana na Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa Mambo ya Nchi za Nje, Ushirikiano pamoja na Mashirika ya Kimataifa.

Rais wa Fiji alikutana pia na viongozi wakuu wa Vatican
Rais wa Fiji alikutana pia na viongozi wakuu wa Vatican

Baba Mtakatifu pamoja na mgeni wake, katika mazungumzo yao ya faragha, wamegusia masuala ya Kimataifa na Kikanda, lakini kwa namna ya pekee kabisa, umuhimu wa kusimama kidete kulinda, kutunza na kudumisha mazingira nyumba ya wote, kwa sababu madhara yake kwa ustawi, maendeleo na mafao ya wengi ni makubwa sana. Viongozi hawa wawili wameridhishwa na uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili pamoja na kuthamini mchango wa Kanisa katika ustawi, maendeleo na mafao ya watu wa Mungu nchini Fiji katika ujumla wao.

Papa Fiji

 

02 August 2022, 15:25