Tafuta

2022.08.15 Santo Domingo.Askofu Mkuu Edgar Peña Parra akikabidhi waridi la dhaabu,ikiwa ni zawadi ya Papa Francisko kwa Mama Yetu wa  Altagracia, huko Jamhuri ya Dominika. 2022.08.15 Santo Domingo.Askofu Mkuu Edgar Peña Parra akikabidhi waridi la dhaabu,ikiwa ni zawadi ya Papa Francisko kwa Mama Yetu wa Altagracia, huko Jamhuri ya Dominika. 

Askofu Mkuu Peña Parra:Inawezekana kufanya kazi kwa umoja

Ushuhuda mkubwa wa imani ya Wadominika iliyosimuliwa kwenye mahojiano ya Televisheni na Katibu Msaidizi wa Vatican na Mwakilishi wa Papa Francisko wakati wa kufunga mwaka wa Jubilei ya Altagracia katika Jamhuri ya Dominika.

VATICAN NEWS.

Nyuma ya kila tendo, kila hati, kila barua, kila uamuzi, kuna Kanisa. Hayo yalilisisitizwa na Askofu Mkuu Edgar Peña Parra, Katibu Msaidizi wa Vatican  na mjumbe wa Papa Francisko katika Jamhuri ya Dominika kwa ajili ya kufunga Mwaka wa Jubilei ya Altagracian, katika mahojiano na Televida, chaneli ya televisheni ya katoliki ya Dominika hivi karibuni.

Misa ya kufunga mwaka wa kuweka taji  la Mama Yesu wa Altagracia iliyoongozwa na Askofu Mkuu Parra huko  Jamhuri ya Dominika
Misa ya kufunga mwaka wa kuweka taji la Mama Yesu wa Altagracia iliyoongozwa na Askofu Mkuu Parra huko Jamhuri ya Dominika

Mwakilishi wa Papa alikumbuka somo moja alilojifunza alipokuwa Padre kijana  alipokuwa anakwenda kwenye balozi: “Ikiwa katika ubalozi inawezekana, kwa kazi ya kujitoa na makini, kwa mfano, kumteua askofu mpya katika jimbo, na askofu nzuri sana, mvuto wa hatua hiyo utakuwa mkubwa sana katika Kanisa na katika nchi anako jikita shughuli yake.

Askofu Mkuu Peña Parra alisisitiza jinsi uteuzi wa mtu sahihi kwa wakati unaofaa, mahali pazuri na kwa njia sahihi, unaweza kubadilisha historia ya jimbo, au ya kiumbe, chochote kile. Pia alieleza kwamba huu ndio umuhimu wa ukweli kwamba, kwa baadhi ya huduma za Kanisa, hata kama zikionekana kuwa za urasimu, Papa huwateua maaskofu ambao wamekuwa na uzoefu wa kidiplomasia, kulingana na ujuzi wao wa ulimwengu na hali halisi mahalia.

Misa ya kufunga mwaka wa kuweka taji  la Mama Yesu wa Altagracia iliyoongozwa na Askofu Mkuu Parra huko  Jamhuri ya Dominika
Misa ya kufunga mwaka wa kuweka taji la Mama Yesu wa Altagracia iliyoongozwa na Askofu Mkuu Parra huko Jamhuri ya Dominika

Alipoulizwa kuhusu uzoefu wake katika Jamhuri ya Dominika, Askofu Peña Parra alishirikisha hisia zake na kusisitiza ushuhuda wa imani ya Wadominika, hasa ibada kwa Bikira Maria wa Altagracia, Mama na Msimamizi wa taifa alisema kwamba anaondoka kwa furaha kwa sababu ameona kwamba inawezekana kufanya kazi pamoja, katika umoja.

Misa ya kufunga mwaka wa kuweka taji  la Mama Yesu wa Altagracia iliyoongozwa na Askofu Mkuu Parra huko  Jamhuri ya Dominika
Misa ya kufunga mwaka wa kuweka taji la Mama Yesu wa Altagracia iliyoongozwa na Askofu Mkuu Parra huko Jamhuri ya Dominika

Ikumbukwe kwamba kila tarehe 21 Januari  inasherehekewa siku kuu ya  Mama Yetu wa Altagracia anayechukuliwa kuwa mama msimamizi  wa kiroho wa watu wa Dominika, na mlinzi wa yote ambayo ni ya Amerika ya Kusini. Alipewa jina la Altagracia kwa sababu hakuna mwingine zaidi yake ambaye ni Mama Mungu anayeweza kutupa watoto wake idadi kubwa ya neema.

30 Agosti 2022, 15:15