Tafuta

2022.05.23 Papa Francisko amekutana na Kiril Petkov, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya  Bulgaria 2022.05.23 Papa Francisko amekutana na Kiril Petkov, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Bulgaria 

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Bulgaria

Jumatatu uwakilishi kutoka nchini Bulgaria ukiongozwa na Waziri Mkuu Kiril Petkov umepokelewa mjini Vatican na Papa Francisko.Ni katika fursa ya mkesha wa Siku ya Watakatifu Cyril na Methodius wanaoheshimika sana nchini Bulgaria kwa elimu na utamaduni wa Kibulgaria na fasihi ya Kislaviki iliyopangwa kufanyika 24 Mei 2022.

Vatican News

Katika mkesha wa Siku ya Watakatifu Cyril na Methodius, watakatifu wanaoheshimika sana nchini Bulgaria kwa elimu na utamaduni wa Kibulgaria na fasihi ya Kislaviki iliyopangwa kufanyika 24 Mei 2022, Jumatatu  asubuhi 23 Mei uwakilishi kutoka nchini humo ukiongozwa na Waziri Mkuu Kiril Petkov umepokelewa mjini Vatican na Papa Francisko.

Papa na Waziri Mkuu wa Bulgaria
Papa na Waziri Mkuu wa Bulgaria

Imekuwa ni zaidi ya robo saa ya mazungumzo ya faragha kati ya Papa Francisko na Waziri Mkuu, ambapo kumekuwapo na nafasi ya kubadilishana zawadi kwa kawaida. Kwa mujibu wa Ofisi ya Vyombo vya Habari Vatican, kwa upande wa Kibulgaria,walileta sanamu za pango zilizotengenezwa kwa vitambaa vya sufu kutoka katika  Kituo cha "Kzaliwa kwa Kristo", kinachohusiana na Kanisa la katoliki la Mitume la Kanisa la Byzantine-Slavic huko Sofia, na Kapeti la Kiutamaduni la Chiprovtsi.

Papa na Waziri Mkuu wa Bulgaria
Papa na Waziri Mkuu wa Bulgaria

Wakati Papa Francisko altoa zawadi ikiwa ni pamoja na nakala ya Ujumbe wa Amani kwa mwaka huu na Hati juu ya Udugu wa Kibinadamu.

Papa na Waziri Mkuu wa Bulgaria
Papa na Waziri Mkuu wa Bulgaria
23 Mei 2022, 16:36